
Tarehe 11 September 2020 –
Washindi wawili wa tuzo za mwaka 2020 za GoGettaz Agripreneur
wametangazwa katika kongamono la Africa Green Revolution Forum Virtual
Summit nchini Rwanda: Moses Katala Mwasisi Mwenza na CEO wa Magofarm
Limited (Tanzania) na Daniella Kwayu Mwasisi Mwenza na CEO wa Phema Agri
(Tanzania). Kila mshindi atapokea dola US$50,000 kwaajili ya kusaidia
na kupanua uendeshaji wa
biashara yao ya kilimo. Kama sehemu ya
Generation Africa youth initiative, lengo la tuzo hii ni kuwaibua na
kuwahamasisha vijana barani Afrika kukamata fursa katika mnyororo wa
thamani wa sekta ya kilimo cha chakula wenye thamani ya $1Tn barani
ndani ya miongo michache ijayo.
Wajasiriamali wengine wanne
vile vile walitajwa kupokea tuzo ya $2,500 ya athari (Impact Award)
Elizabeth Gikebe, Mwasisi na CEO wa Mhogo Foods (Kenya), Millicent
Agidipo, Mwasisi mwenza na Meneja Uzalishaji wa Achiever Foods (Ghana),
Dysmus Kisulu, Mwasisi mwenza na CEO wa Solar Freeze (Kenya) na Paul
Matovu,Mwasisi na CEO wa Vertical Farm and Micro-Gardening (Uganda).
Wajasiriamali hawa walichaguliwa na majaji kwa kuonyesha athari chanya
katika mazingira au kwa jamii wanazotokana na biashara zao, kila mmoja
akiwa anajitahidi kufikia malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo
Endelevu na kunufaisha jamii zao. Wajasiriamali wote 12 walioingia
fainali na watapata ushauri, kuunganishwa na programu pamoja na kupata
miongozo ya kuendelea na safari yao ya ujasiriamali.
Mashindano ya pili ya mwaka
2020 ya tuzo ya GoGettaz Agripreneur Prize yaliaanza mwezi Aprili na
kwisha mwezi Juni mwaka huu. Zaidi ya waombaji 3000 wa kati ya umri wa
miaka 18 hadi 35 kutoka katika nchi 29 wamejiandikisha kushindana. Japo
kuwa utofauti wao umeshika mnyororo mzima wa thamani wa kilimo cha
chakula kutokea katika uzalishaji wa msingi mpaka katika uvumbuzi wa
teknolojia za kidigitali, Vijana wote sita wa kike na vijana sita wa
kiume ni wajasiriamali kutoka katika nchi tisa za kiafrika ambao
wamefanikiwa kuingia katika 12 Bora walikuwa wanafanana japo katika kitu
kimoja: waliona tatizo na kufanya mipango mikubwa kutatua changamoto
hizo kwa kuanzisha kampuni mpya katika sekta ya kilimo cha chakula
Afrika.
Wajasiriamali na miradi
iliyoingia fainali ya 12 Bora mwaka huu wanatokea Ghana, Kenya, Malawi,
Morocco, Nigeria, Rwanda, Sierra Leone, Afrika ya Kusini, Tanzania na
Uganda.
Katika shindano la kunadi wazo
wakati wa fainali mapema wiki hii washiriki wote walioko fainali
waliwasilisha mawazo yao moja kwa moja kupitia mtandao kwa dakika tatu
mbele ya majaji nane ambao walikuwa na dakika mbili za kuuliza maswali.
Hiki hapa ndio kiungo (Link) kukuwezesha kutazama shindano la kunadi
wazo ambalo lilikuwa linatangazwa ulimwenguni kote katika mkutano wa
AGRF na katika mitandao ya kijamii tarehe 8 Sept 2020. https://www.facebook.com/GoGettazAfrica/videos/645057906424901
Kwa mwaka huu majaji 8 (tazama hapa chini) waliwatathmini waasisi wa biashara pamoja na mradi kwa kuzingatia vigezo vitano:
- Uvumbuzi
- Mfumo wa Biashara
- Athari kwa Jamii na Mazingira
- Uwezo wa kuvutia Soko
- Timu ya Usimamizi
Ili kuweza kuingia katika 12
Bora kila mshiriki aliyeko fainali alipaswa kuwasilisha ombi kwa mtandao
lenye maelezo kwa upana kabla ya kufikia June. Washiriki 24 wa kwanza
waliochaguliwa kuingia nusu fainali baada ya hapo walipaswa kutengeneza
video yao wenyewe ya kueleza wazo na kushiriki katika mahojiano ya
dakika 30 na jopo la majaji kupitia mtandao
“Katika kipindi chote cha
changamoto ya Covid cha mwaka 2020, GoGettaz agripreneurs iliendelea
kuwa makini na yenye msukumo, sio wakiwa wanajali tu biashara yao na
wafanyakazi lakini pia nchi zao na wananchi wenzao pia. Katika
kukabiliana na janga la kimataifa walianza kutumia mfumo mpya
kukabiliana na mahitaji na changamoto mpya,” Alisema Dickson Naftali,
Mkuu wa Generation Africa initiative aliyeko Nairobi. “Washiriki 12
walioingia fainali mwaka huu tayari wana nguvu ya msukumo kwaajili kukua
na kuleta mabadiliko katika jamii zao. Biashara zao za kilimo kila
mmoja iko tofauti, lakini wote wanachochea bara la Afrika kuwa lenye
nguvu katika kilimo”.
WASHINDI WA TUZO YA US$50,000 YA GOGETTAZ AGRIPRENEUR MWAKA 2020
Daniella Kwayu, mwasisi mwenza na CEO wa Phema Agri nchini Tanzania. www.phemaagri.com
Phema Agri ni jukwaa la
kidigitali la kilimo linalounganisha wawekezaji wanaotaka kukuza fedha
zao kwa kupitia wakulima wadogo wadogo wanaotafuta mitaji ya kufanyia
kazi. Kwa kupiti mfumo wao wa crowdfunding (www.phemaagri.com) Taasisi
ya Phema Agri iliwaunganisha, iliwaondolea hatari, kuwachumguza na
kuwaunganisha na masoko wakulima wanaotafuta wawekezaji. Mwisho wa siku
wakulima wanagawana faida na wawekezaji wao. Mfumo huu unafuata mtindo
wa biashara wa B2B2C ambao umeunganishwa moja kwa moja na malipo ya
banki pamoja na waendeshaji wa simu za mkononi kurahisisha miamala.
“Pengo la kuwezesha kifedha
sekta ya kilimo barani Afrika ni US $150 billion kama ilivyokuwa mwaka
2019,” alifafanua Daniella katika maombi yake kwa njia ya mtandao.
“Hakuna washindani wa moja kwa moja kwa jukwaa la kilimo nchini
Tanzania. Sisi ni taasisi ya kwanza sokoni katika sehemu hii ya sekta.
Uwekezaji katika kilimo. Utofauti wetu mkubwa ni uwezo wetu wa kutumia
teknolojia kuleta masoko yaliyoundwa kwa usalama, uwekezaji ulioratibuwa
vyema kwa njia ya kawaida.”
Phema Agri inakusudia kufikia
malengo yake ya kuwawezesha kifedha wakulima milioni moja na kudhibiti
minyororo mitano ya thamani katika soko la Afrika Mashariki. Kwa sasa
Phema Agri wanafanya kazi katika minyororo miwili tu ya thamani
(Minyororo ya thamani ya kuku na nguruwe) wakiwa na lengo la kuongeza
thamani zingine za (mahindi, Viazi, Ngano) na kuwapa mafunzo wakulima
wengi zaidi kuhusu thamani hizi. Msaada huu wa kifedha kutoka kwenye
tuzo za GoGettaz Agripreneur 2020 zitatumiwa kujipatia mikataba ya
masoko na tathmini za masoko kwa lengo la kuweka mifumo na kuunganisha
wakulima wengi zaidi.
Moses Katala, mwasisi mwenza na CEO wa Magofarm Limited, Mtanzania anayeishi nchini Rwanda. www.magofarms.com
Magofarm Limited inakusudia
kutatua changamoto ya gharama zinazoongezeka za vyakula vya mifugo na
ongezeko la mahitaji ya upatikanaji endelevu wa viungo vyenye protini na
visivyo na athari kwenye uchumi Kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la
kushughulikia chakula na kilimo (FAO), wafugaji wa kuku kibiashara
Afrika wanakumbana na ongezeko la asilimia 20% la bei ya vyakula vya
mifugo chenye soya beans na fishmeal kama chanzo cha viungo vyenye
protein. Kwa sasa viungo vyenye protein sokoni sio tu kwamba ni ghali
kuzalisha lakini pia mzunguko wa uzalishaji wake unaweza kuwa na athari
kubwa kwenye mazingira, alibainisha Katala katika maombi yake ya hatua
ya kwanza.
“Vile vile tuko katika azimio
la kupunguza upotevu wa chakula katika nchi zinazoendelea,” Alisema
Katala. “Upotevu wa chakula una wakilisha upotevu wa rasilimali kama
vile ardhi, nishati, maji na vitendea kazi, na hatimae kupelekea katika
uzalishaji wa gesi ya ukaa usiyo wa lazima. Kwa mujibu wa FAO, ingekuwa
upoteaji wa chakula ni nchi, basi ingekuwa ni nchi ya tatu kwa
uzalishaji mkubwa zaidi wa gesi ya ukaa duniani baada ya China na USA.
Dunia inahitaji suluhisho endelevu la kukabiliana na uharibifu wa
chakula. Gharama za kila mwaka za chakula kinachoharibika duniani
kinakadiriwa kufika $990 billion”.
“Kwa kuzalisha black soldier
fly larvae, Magofarm imejipatia uwezo mkubwa sana wa kupunguza uharibifu
wa chakula. Kwa kila tani moja ya black soldier fly larvae tunayozasha
kutumia tani 3 za taka za chakula kutoka katika mazingira, ambazo sisi
tunazitumia kama malighafi. Kwa kila tani ya fishmeal na Soymeal
inayookolewa kutokana na kutumiwa kwa protein zitokanazo na wadudu
(magomeal), utunzaji wa mazingira wa kati ya $2,500 na $3,200 kwa kila
tani inafikiwa kwa njia ya kuepuka matumizi ya mafuta, matumizi ya
ardhi na uzalishaji wa gesi ya ukaa”.
WASHINDI WA $2,500 – TUZO YA ATHARI
Elizabeth Gikebe, Mwasisi mwenza na CEO, Mhogo Foods
Ltd inchini Kenya: Mhogo Foods ni taasisi ya ufahamu wa jamii ya
kuchakata muhogo na kutengeneza unga wa mhongo usio na gluteni, crisps,
wanga na vyakula vya mifugo wakati huo huo ikiwa inatoa mafunzo na
kuwasaidia wanawake wanaojihusisha na kilimo kwa kiwango kidogo.
www.mhogofoods.com
Millicent Agidipo, mwasisi mwenza na CEO of Achiever Foods Limited
inchini Ghana: Achiever Foods iko katika mkakati wa kuokoa maisha kwa
kupitia kilimo cha kisasa au cha kioganiki cha Turkey Berries ambazo
hutumika kukuza afya ya damu na kuimarisha mfumo wa kinga hasa miongoni
mwa wanawake wajawazito. www.achieverfoods.net/en/
Paul Matovu wa Vertical and Micro Gardening (VMG)
inchini Uganda: VMG inajenga mashamba ya kujiendesha yenyewe kwa lengo
la kufanya kilimo cha mijini kuwa chenye faida kwaajili ya familia zenye
kipato cha chini na cha kati . www.verticalandmicrogardening.org
Dysmus Kisilu mwasisi mwenza na CEO Solar Freeze
inchini Kenya: Solar Freeze inasaidia kupambana na kuharibika kwa mazao
baada ya kuvunwa na wakulima wadogo wadogo wa bidhaa zinazooza kwa
haraka kwa kutumia vifaa vya solar vya kuhifazia vyenye baridi na
“sharing economy” vifaa mbalimbali vya baridi vya kihifadhia.
www.solarfreeze.co.ke
Washiriki wengine 12 wa kwanza wa tuzo ya GoGettaz Agripreneur mwaka 2020:
Fadja Dijou Barry, GoMarkit SL, Sierra Leone. www.gomarkitsl.com
Dexter Tangocci, Integrated Aerial Systems, South Africa. www.iasystems.co.za
Kharbouch Barhoum, Lombrisol, Morocco. www.lombrisol.ma
Brigitha Faustin, Obri Tanzania. www.obritanzania.com
Ifeoluwa Olatayo, Soupah Farm-en-Market Ltd., Nigeria. www.soupah.ng
Agnes Kanjala, The Farm, Malawi. www.thefarmmw.com
JOPO LA MAJAJI 12 WA JUU WA TUZO YA GOGETTAZ AGRIPRENEUR
Eleni Gabre-Madhin
Mwasisi & Afisa Mkuu wa Furaha, bluMoon
Generation Africa Ambassador
Ada Osakwe
Mwasisi & CEO, Agrolay Ventures Nigeria
Generation Africa Ambassador
Generation Africa Ambassador
Ishmael Sunga
CEO, Southern African Confederation of Agricultural Unions
Generation Africa Ambassador
Generation Africa Ambassador
Ellen Cathrine Rasmussen
EVP wa Scalable Enterprises, Norfund
Edson Mpyisi
Mchumi Mkuu wa Fedha & Mratibu wa ENABLE Youth Program, Benki ya Maendeleo ya Afrika (African Development Bank)
Ladé Araba
Mkurugenzi Mtendaji wa Afrika, Convergence Finance
Mwasisi mwenza/Rais wa taasisi ya Visiola Foundation
George Apaka
Lead Agriculture Sector, Mastercard Foundation
Lead Agriculture Sector, Mastercard Foundation
Zvichapera Katiyo
Group CEO, Delta Philanthropies, Zimbabwe
WAASISI WENZA NA WASHIRIKA WA KIUFUNDI
Mwaka 2019 international technology group Econet pamoja na global crop nutrition leader Yara,
kwa pamoja wali chochea kukua kwa Generation Africa initiative kwa
dhumuni la kuwahamasisha na kuwasaidia vijana wajasiriamali wa kilimo
Africa na kuleta pamoja taasisi zenye upeo, mashirika na taasisi
zinazoshughulika na vijana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya kilimo
cha chakula Afrika.
Mafanikio ya kampeni ya
GoGettaz Agripreneur Prize iliyozinduliwa Davos mapema mwaka 2019
yaliwavutia viongozi wengine katika sekta ya kilimo ulimwenguni na
Afrika Mnamo mwaka 2020 Generation Africa initiative iliongeza
washirika wengine wanne katika timu yake ya wenye maono: The Alliance for a Green Revolution in Africa (AGRA), Corteva Agriscience, the Southern African Confederation of Agricultural Unions (SACAU) na the Syngenta Foundation for Sustainable Agriculture.
No comments :
Post a Comment