Shule
ya sekondari Simiyu ni miongoni mwa shule nufaika na mikakati
inayofanywa na shirika lisilo la kiserikali la world vision, ambapo jana
imepokea msaada wa vitanda 50 (double decker) pamoja na magodoro 100.
Akikabidhi
vitanda hivyo kaimu meneja wa krasta ya Nzega Gilselda Balyagati
alisema, Kupitia mradi wa KANADI shirika limeweza kutoa milioni 26.6 kwa
ajili ya kuhakikisha kuwa linamtengenezea mtoto wa kike mazingira
mazuri ya kupata elimu.
"Lengo
la shirika ni kuwalinda wasichana dhidi ya vishawishi pamoja na mimba
na ndoa za utotoni na kuhakikisha kuwa wanapata elimu bora," alisema
Aliongeza
kuwa, wanaishukuru serikali kwa ushirikiano inao utoa kwa mashirika
binafsi na wadau wengine wa maendeleo hali inayowafanya wasichoke kuunga
mkoa sera ya serikali ya hapa kazi tu.
Akipokea
vitanda hivyo mkuu wa wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga alisema kuwa, ni
wakati wa wanafunzi kutumia fursa wanazosogezewa na serikali kwa ajili
ya manufaa yao na kiacha kucheza na wakati.
"Nyinyi
kazi yenu ni kusoma tu, sitarajii kuwa serikali ikufanyie kila kitu na
ufeli huo utakuwa ni ujinga wako wekeza sana katika kusoma maana elimu
inatolewa bure," alisema Kiswaga.
Kiswaga
aliongeza kuwa licha ya upatikanaji wa wadau katika kusaidia kuboresha
Elimu Walimu pia wanajukumu kubwa kuhakikisha kuwa wanafanya kazi
ipasavyo ili kuwawezesha wanafunzi kifauru vizuri.
Aidha
baadhi ya wanafunzi ambao ni wanufaika wa msaada huo, wameeleza namna
ambavyo wamepokea vitanda hivyo na kusema kuwa kwao ni mafanikio makubwa
katika elimu.
"Ukilala
vizuri lazima uamke akili yako imechangamka tumefurahi sana na sisi
tunaahidi kutunza vizuri vitanda na magodoro haya ili hata wadogo zetu
waweze kuyatumia hapo baadae," alisema Kwiyeya Lameck Buluba mwanafunzi
wa kidato cha kwanza.
"Ni
faraja kwetu tunapoona kunawatu wapo nyuma yetu ili kuhakikisha
tunapata elimu bora na kulindwa dhidi ya ukatili wa kingono, tumepata
vitanda vingi ambavyo vitatusaidia kuishi mazingira ya hapo shuleni ni
jambo la kushukuru sana," alieleza Rita Masunga mwanafunzi wa kidato cha
tatu.
Shirika
la world vision Tanzania ni miongoni mwa mashirika yasiyo ya kiserikali
ambayo yamekuwa na mchango mkubwa katika kuleta maendeleo kwenye jamii
hasahasa katika upande wa Elimu na Afya.
No comments :
Post a Comment