Wednesday, August 12, 2020

NAIBU WAZIRI SIMA AKAGUA KIWANDA CHA TBL MBEYA


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima akipata maelezo ya shughuli za uendeshaji wa Kiwanda cha Bia Mbeya kutoka kwa Bw. Emmanuel Sawe  Meneja Mkuu wa Kiwanda hicho. Kushoto  ni Prof Esnat Chaggu Mwenyekiti wa Bodi – Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC.

Meneja uzalishaji Kiwanda cha Bia Mbeya Bw. Misana Misana akifafanua jambo kwa  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima katika ziara ya ukaguzi  kiwandani hapo. Kushoto ni Prof Esnat Chaggu Mwenyekiti wa Bodi – Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC na wa kwanza kulia ni Dkt Samuel Gwamaka Mkurugenzi Mkuu – NEMC

Dkt. Samuel Gwamaka Mkurugenzi Mkuu, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira – NEMC akisisitiza jambo kwa watendaji wa Kiwanda cha Bia cha Mbeya baada ya ziara ya kikazi kiwandani hapo kuangalia uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira.

No comments :

Post a Comment