Wednesday, August 12, 2020

DK.SHEIN AKUTANA NA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  (kushoto) akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Fedha na Mipango  katika kikao cha Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha Mwaka 2020/2021 kilichofanyika jana katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Mohamed Ramia Abdiwawa akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji mpango kazi wa mwaka 2020/2021 katika kikao kilichofanyika jana katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar(kushoto) Mshauri wa Rais Uwezeshaji na Uwekezaji Bw.Abdulrahman Mwinyi Jumbe na Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Abduhamid Yahya Mzee.

Viongozi wa Idara mbali mbali katika Wizara ya Fedha na Mipango  wakiwa katika Kikao cha Utekelezaji Mpango kazi wa Mwaka 2020/2021 kilichofanyika jana katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  (hayupo pichani).

Baadhi ya Viongozi wa Idara mbali mbali katika Wizara ya Fedha na Mipango wakiwa katika Kikao cha Utekelezaji Mpango kazi wa Mwaka 2020/2021 kilichofanyika jana katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  (hayupo pichani).

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Nd,Khamis Mussa Omar akitoa shukurani kwa niaba ya Wafanyakazi na Viongozi wa Wizara kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  (hayupo pichani) kwa Uongozi wake wakati wa Kikao cha Utekelezaji Mpango kazi wa Mwaka 2020/2021 kilichofanyika jana katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar.

 MSHAURI wa Rais Pemba Dk.Mauwa Abeid Daftari alipokuwa akichangia katika kikao cha Uongozi wa Wizara ya Fedha na Mipango cha Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha Mwaka 2020/2021 kilichofanyika jana katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar (kulia) Mshauri wa Rais Uwezeshaji na Uwekezaji Bw.Abdulrahman Mwinyi Jumbe, [Picha na Ikulu.

No comments :

Post a Comment