********************************
Mwandishi Wetu, Mwanza
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana
Mkoani Mwanza Mhe. Dr.Phillis Nyimbi amesema masuala ya usalama na afya
kwa wajasiriamali ni muhimu, kwani kutokuzingatia kwake kuweza kuleta
athari kwa mfanyakazi na hivyo kutaathiri jamii na taifa kwa ujumla
Mhe. Nyimbi amesema hayo wakati
akifungua Semina maalumu kwa wajasirimali wadogo na wakati ,Semina ya
usalama na afya yalioyoandaliwa na OSHA kwa kushirikiana na SIDO mkoa wa
Mwanza, Semina iliyofanyika Jijini Mwanza. Amesema endapo tahadhari
haitachukuliwa, itawasababishia madhara makubwa na hivyo kuwa mzigo kwa
jamii na taifa kwa ujumla.
Mkuu huyo wa Wilaya amengeza na
kusema, wakati mwingine ni kutokutilia maananini kwa baadhi ya watu, na
kuacha kununua vifaa vya kuwakinga wakati wakiwa kazini na hivyo
kuchangia hatari ya kuweza kupata madhara wakati wakiendelea na kazi.
“Lakini pamoja na hayo, tukumbuke kwamba, suala la usalama na afya nijukumu letu sote, magonjwa na
ajali zinazotokea sehemu za kazi,
mara nyingi zina athari nyingi sio kwetu tu, bali hata kwa jamii, Vifaa
mnavyotumia, wengine mnatumia kemikali katika uzalishaji wa bidhaa
zenu, hii kwa kiasi kikubwa zinaweza zikaleta madhara makubwa kwenu
nyinyi na hata wale watakaokwenda kutumia endapo hatua madhubuti
hazitachukuliwa, madhara yake yanaweza yakawa makubwa sana, hivyo
matumizi sahihi ya vifaa kinga ( PPE) katika kazi zenu hayaepukiki. “
Aliongeza Dr. Nyimbi
Kwa upande wake Mkurugenzi wa
mafunzo,Utafiti,na Takwimu, Ndugu Joshua Matiko, amesema wajasiriamali
wanakabiliwa na changamoto mbalimbali na hivyo kuwataka kila wanapokuwa
wanafanya shughuli zao wazungumzie masuala ya usalama na afya kabla ya
kuanza kazi, ili kubainisha vihatarishi vinavyopatikana kwenye maeneo
yao kazi, unajaribu kuzungumza kuna namna ya kuviepuka .
“ Kuna haja ya kuweka mabango
yatakayosaidia kutukumbusha masuala ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi,
na hivyo kuchukua tahadhari kwenye maeneo yetu ya kazi” alielezea
mkurugenzi wa mafunzo,
Kwa upande wao washiriki wa
mafunzo hayo, wamesema semina hiyo imewajengea msingi mzuri wa kuweza
kufanya shughuli zao za uzalishaji huku wakichukua tahadhari ya kufanya
kazi katika mazingira salama na kulinda afya zaa.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi
kufungua semina hiyo, Meneja wa SIDO mkoa wa Mwanza Ndugu Bakari Songwe
amesema, SIDO kama taasisi wezesheji kwa wajasiriamali amesema waliona
umuhimu wakuwashirikisha OSHA ili waweze kutoa semina ya kuwawezesha
wajasirimali hao namna bora ya kufanya kazi huku wakizingatia Usalama na
Afya wakiwa kazini.
Mafunzo haya yamefanyika katika
mkoa wa Dodoma na sasa Mwanza ambayo yanalenga kuwajengea uwezo
wajasiriamali wadogo namna bora ya kulinda usalama na afya kwa wadau wao
ambao wanamchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi.
No comments :
Post a Comment