Tuesday, June 9, 2020

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI JENERALI MABEYO AIPONGEZA RTS KIHANGAIKO KUENDESHA MAFUNZO NA MIRADI



Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo akikagua paredi maalum la askari wapya kundi 39/20 waliohitimu mafunzo ya uaskari katika Chuo cha Mafunzo ya awali RTS-Kihangaiko, Msata Mkoani Pwani.(Picha na Luteni Semunyu)
Baadhi ya Askari wapya wanawake kundi 39/20 wakiwa katika picha ya pamoja na mmoja wa waliovalishwa Medali kwa kufanya vizuri wakati wa  kufungwa mafunzo ya awali ya kijeshi katika Chuo cha Mafunzo RTS-Kihangaiko, Mkoani Pwani.( Picha na Luteni Selemani Semunyu)
Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo akimkabidhi zawadi mwanafunzi aliyefanya vizuri katika mafunzo ya awali katika chuo cha mafunzo ya awali RTS-Kihangaiko Picha na Luteni Selemani Semunyu.
Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo akikata utepe kuzindua Mradi wa maji katika chuo cha mafunzo ya awali RTS-Kihangaiko Picha na Luteni Selemani Semunyu.
******************************
Na Luteni Selemani Semunyu
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini  Jenerali Venance Mabeyo amepongeza chuo Cha mafunzo ya awali ya Kijeshi cha RTS Kihangaiko kutokana na usisimamizi wa mafunzo na Ujenzi wa
Miradi ya  kujitegemea.
Jenerali Mabeyo alisema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa sherehe za kuapa kwa Askari wapya kundi la 39 katika chuo hicho kilichopo Msata Bagamoyo Mkoani Pwani.
“Sina Shaka na mazoezi mliopatiwa na nimeshuhudia pia kupitiaa vyombo vya habari mlipokuwa mkihitoimisha mafunzo ya Porini mnastahili pongezi” Alisema Jenerali mabeyo
Alisema kufanya zoezi la pamoja kwa kujumuisha vikosi mbalimbali tena kwa kutumia gharama za shule ni hatua kubwa ya kupongezwa.
Aliongeza kuwa anafurahi kuona Askari wapya mbele yake kwani ni ishara kwamba wameiva wako imara katika kutumikia JWTZ lakini pongezi kubwa ni kwa wakufunzi waliohakikisha wanafika  hatua hiyo.
Aidha aliwataka askari wapya kuhakikisha wanalinda nchi  kwa uadilifu kwani ndio jukumu lao kubwa na kuwa waadilifu kwa kuishi kiapoa chao.
” Muhakikishe mnaishi kiapo chenu na muwe tayari kutekeleza majukumu hayo mahala popote  bila kuchagua kwani jeshi ndio linajua wapi mnaweza kutumika, Alisema Jenerali Mabeyo.
katika hatua nyingine aliwataka watu wote wenye jambo au masuala na jeshi hilo kutozunguka wafuate utaratibu wa kijeshi badala kutaka kuwatumia viongozi wengine wakati Mkuu wa majeshi na wasaidizi wake wapo.
” Usifikiri ukimueleza Rais shida yako ukadhani haitorudi kwetu au ukimweleza Waziri au ukinieleza mimi ndio litashughulikiwa haraka tufuate utaratibu, Alisema Jenerali Mabeyo.
Kuhusu Miradi alisema ipo haja ya jeshi la wananchi kuendelea kuweka jitihada katika miradi yao wenyewe ili kuepusha adha mbalimbali na matumizi yasiyo ya lazima.
Kwa upande wake kaimu Mkuu wa shule ya mafunzo ya awali RTS Kihangaiko Kanali Sijaona Myala alisema askari waliohitimu ni 3575 wanaume  wakiwa 3245 na wanawake ni 330 huku 11 wakipoteza maisha wakati wa Mafunzo.
Aliongeza kuwa wamejifunza mambo mbalimbali kulingana na silabi ya mafunzo huku akisema mambo manne muhimu wanayotakiwa kuyafanya wawapo jeshini muda wote ni utii, uaminifu, na Uhodari.
“Mna dhamana kubwa sana ndani ya jeshi, dhamana hii mkaitumie vizuri, jiepusheni na migogoro baina yenu na raia ikiwa ni pamoja na kujichukulia hatua mikononi” Alisema kanali Myala.
Awali mkuu wa kamandi ya Vikosi Chini ya makao Makuu ya Jeshi Meja Jenerali Sharif Othman alisema ameshuhudia uimaraa wao na ana matumaini makubwa na Askari hao.

No comments :

Post a Comment