![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhbiQLm3YvNBORPCMfkIlJDm5MeYEEXUla4akEUe0Ucar2I2KfuAHefzOOvVJBbVdjTtzmPVtTsj-dcTYsXWHhOAYar8iSMYjBfd4QlEWGy0Fmz3dKR72Wu8d1WHGSiiyzRD1NTfYPjlG4B/s640/41703274_303.jpg)
Katika ujumbe huo Rais aliandika “Ndugu
zangu Watanzania, kutokana na ugonjwa wa Corona, nawaomba tutumie siku 3 za
kuanzia tarehe 17- 19 Aprili, 2020 {Ijumaa, Jumamosi na Jumapili} KUMUOMBA
MWENYEZI MUNGU aliye muweza wa yote atuepushe na janga la ugonjwa huu. Tusali
kwa kila mmoja kwa imani yake, atatusikia”.Aliandika Rais Magufuli.
Ugonjwa wa COVID-19 ama Virusi vya CORONA
ulianzia jimnbo la Wuhan nchini China Desemba mwaka 2019 na kutapakaa dunia
nzima ambapo tayari umesababisha maafa makubwa.
Hadi
kufikia Alhamisi Aprili 16, 2020, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu alisema, tawimu zinaonyesha hadi sasa kuna jumla ya
wagonjwa wa CORONA 94 na amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kwa
kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka mara kwa mara, kuepuka mikusanyiko
isiyo ya lazima.
No comments :
Post a Comment