Timu ya mbio za magari kutoka Mkwawa chini ya Ahmed Huwel
wakionyesha vikombe vya ubingwa walivyobeba katika moja ya mashindano ya
magari .
Mkuu wa mkoa wa Iringa akimpongeza Ahmed Huwel ‘Simba’ katika moja ya mashindano aliyochukua ubingwa wa kukimbiza magari.
…………………………………………………………………
NA DENIS MLOWE,IRINGA
KLABU ya Mbio za Magari mkoa
wa Iringa(Iringa Motorsport Club Tanzania)imejipanga kurudi vyema msimu
mpya unaotarajiwa kuanza hivi karibuni katika kuinua mchezo wa
kukimbiza magari nchini na kutoa bingwa wan chi kutoka ndani ya klabu
hiyo.
Akizungumza na mwanahabari
hizi,Mwenyekiti wa Klabu hiyo mkoa wa Iringa, Hamid Mbata alisema kuwa
wamejipanga vyema kuweza kuinua mchezo huo kwa mkoa wa Iringa na nchini
kwa ujumla kwa kuwa wana wanachama wenye moyo na nia ya kufanya hivyo
kwenye mchezo huo.
Mbata alisema kuwa kwa
wanachama wa Klabu hiyo mkoa wa Iringa wamekuwa mstari wa mbele katika
kulipia ada ya mwaka ya uanachama hali ambayo itawezesha kushiriki
mashindano mbalimbali na kuendelea kuifanya klabu kuwa hai zaidi.
Klabu hiyo yenye wanachama
mbalimbali akiwemo bingwa wa magari nchini Ahmed Huwel na mkuu wa wilaya
ya Iringa Richard Kasesela ndio klabu ambayo imekuwa mstari wa mbele
katika kuandaa mashindano ya magari nchini yakiwemo ya Mkwawa Rally
ambayo yamejizolea umaarufu nchini kwa sasa na kudhaminiwa na maji ya
Mkwawa.
Aliwataka wanachama kuendelea
kulipia ada za klabu kama ambavyo wengine wametoa ada zao kwa mwaka
mzima na wanaruhusiwa kulipia kipindi cha nusu mwaka ambapo kwa miezi 6
wanalipia sh. 30000 ambacho kinaishia mwezi Juni mwaka huu na ada ya
mwaka mzima ni 60000 na kulipia 10000 ya kitambulisho.
Alisema kuwa kwa sasa chama
hicho kimeweka mikakati ya kufanya vyema mkoani hapa na nchini kwa
ujumla hali ambayo inatokana na ushirikiano mzuri na wanachama wa klabu
hiyo ambayo wengi wamekwa wakishiriki mashindano mbalimbali ya ndani na
nje ya nchi yanayojitokeza.
Mbata ambaye ni mshiriki wa
mashindano yanayofanyika nchini akiwa chini ya msoma ramani wake Sultan
Chana amewashukuru wanachama wa Iringa Motorsports Club kwa michango yao
mbalimbali ndani ya klabu hiyo na kuwataka kuungana katika kujiandaa
na msimu mpya wa mashindano.
Klabu hiyo yenye wanachama 34
baadhi yao wakiwa ni wafanyabiashara wakubwa mkoani hapa, na wanachama
wa kada mbalimbali akiwemo mwanasheria maarufu mkoani hapa Barnabas
Nyalusi, Mkurugenzi wa uzalishaji wa kampuni ya Asasa Ahmed Salim na
mchezaji wa zamani wa Yanga Ally Msigwa.
No comments :
Post a Comment