……………………………………………………………………………………..
Na.Alex Sonna,Dodoma
Bunge limeelezwa
kuwa ,Kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na Wizara ya Madini katika
kutenga maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo na kufungua masoko ya
madini nchi nzima, kumesababisha ongezeko la wachimbaji wadogo ambao
wamekuwa wakivamia maeneo
mbalimbali ya Migodi midogo (rush) .
Taarifa hiyo
imetolewa leo Bungeni jijini Dodoma kutoka wizara ya Madini kwa njia
ya Maandishi wakati Wizara hiyo ikijibu swali la Mbunge wa viti
Maalum Salome Makamba aliyehoji Je, ni sifa zipi ambazo mzabuni
anatakiwa kuwa nazo ili kupewa nafasi ya usimamizi mapato ya Serikali
kwenye migodi midogo midogo (Rush) kama Mwabomba, namba Mbili, Segese.
Katika Majibu ya
Wizara ya Madini imefafanua kuwa maeneo ambayo yanavamiwa zaidi na
wachimbaji wadogo ni yale yaliyotengwa, maeneo yenye leseni kubwa za
utafiti, maeneo ya uchimbaji mkubwa, maeneo yasiokuwa na leseni, na
maeneo ambayo leseni zake hazijaendelezwa kwa shughuli za uchimbaji.
Aidha Majibu ya
wizara hiyo yameendelea kufafanua kuwa ,Serikali kupitia Tume ya Madini
ilitoa Waraka wa Ndani Na. 3 ulioanza kutumika tarehe 15 Oktoba, 2019
wenye dhumuni la kutoa mwongozo kwa Maafisa Madini Wakazi na watumishi
wengine katika kusimamia, kudhibiti shughuli za madini na mapato ya
Serikali katika maeneo yenye Migodi midogo[rush.]
Kwa mujibu wa
Waraka huo, utaratibu unaotumika kuwapata wasimamizi wa rush ni kupitia
Kamati ya Uongozi inayofuatilia na kuimarisha usimamizi katika eneo la
rush.
Majibu ya Wizara
ya madini yameendelea kubainisha kuwa ,Kamati hiyo huteua Wasimamizi wa
migodi midogomidogo[ rush], ambapo Mwenyekiti wa rush anapaswa kuwa na
sifa zifuatazo:- Awe mchimbaji mzoefu hasa katika usimamizi wa maeneo ya
aina hiyo; Asiwe na historia ya wizi wa fedha za Serikali; na Awe
mwaminifu.
Aidha, wajumbe
wengine kwenye usimamizi wa rush ni pamoja na Katibu, Mweka Hazina,
M/kiti wa Kijiji, M/kiti wa Kitongoji, Mjumbe wa REMA, TAWOMA na
Mwakilishi wa eneo/shamba.
No comments :
Post a Comment