Friday, March 6, 2020

ZOEZI LA KUWAHAMISHA VIBOKO BWAWA LA MILALA LIMEKWAMA



Naibu Waziri wa Mali Asili na Utalii Constantine Kanyasu (mrefu kuliko wote) kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda mama Lilian Matinga; wakiwa pembezoni mwa bwawa la Milala
Mmoja wa wanyama aina ya kiboko wanaolalamikiwa na wananchi wa kata ya Misunkumilo kwa uharibifu wa mazao 
……………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi wetu, Katavi
Zoezi la kuwahamisha wanyama pori aina ya viboko wanaoishi katika bwawa la Milala manispaa ya Mpanda mkoani Katavi limeendelea kukwama kutokana viboko hao kukimbilia
katika mito midogo baada ya maji kujaa katika bwawa hilo kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha 

Akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Mali Asili na Utalii aliyefanya ziara mkoani Katavi; Mtafiti wa wanyama pori kutoka Taasisi ya Wanyama Pori ya TAWIRI Dk. Emmanuel Masenga amesema zoezi hilo limesitishwa mpaka wakati wa kiangazi
Dk. Masenga ameeleza kuwa kwa sasa viboko hao wamehamia katika mito midogo midogo inayojaza maji katika bwawahilo ambapo ni vigumu kuwaondoa
“Kule hakuna barabara, na kama tukitaka kuwatoa huko tutafanya uharibifu mkubwa kwa mazao ya wananchi” alisema Dk. Masenga
Ameendelea kuelea kuwa kiboko ana uwezo wa kutembea umbali wa kilometa kumi kwa siku hivyo hata wakiondolewa wana uwezo wa kurudi katika bwawa hilo na hivyo kupendekeza kujengwa kwa uzio kuzunguka bwawa pamoja na kuweka askari wanyama pori kwa ajili ya kulinda eneo hilo

Bwana Iddo Richa ni mhandisi kutoka Mamlaka ya Maji Mpanda, ambao ndio wasimamizi wa bwawa hilo, amlisema wanahitaji kiasi cha shilingi bilioni moja nukta mbili ili kujenga uzio kuzunguka bwawa hilo
Hata hivyo alisema fedha hizo ni nyingi na hawawezi kuzipata kupitia makusanyo yao hivyo kuomba serikali kuu kuangalia uwezekano wa kusaidia
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mali Asili na Utalii mheshimiwa Constantine Kanyasu amewatoa wasiwasi wananchi wanaoishi katika maeneo hayo na kuahidi serikali itatafuta fedha za kujenga uzio

No comments :

Post a Comment