Friday, March 6, 2020

Waziri Mwakyembe apokea ripoti ya utekelezaji wa mkataba wa UNESCO 2005.


Mratibu wa Kitaifa wa utekelezaji wa mkataba wa UNESCO 2005 Bw. Boniface Kadili (wa pili kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na
Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) Wakati wa kukabidhi taarifa ya utekelezaji wa mkataba huo mapema hii leo 6Machi katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es
Salaam.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akisoma taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa UNESCO 2005 mara baada ya kuipokea
mapema hii leo 6 Machi katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akimsikiliza Mratibu wa Kitaifa wa utekelezaji wa mkataba wa UNESCO 2005 Bw. Boniface Kadili Wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa huo mara baada ya kuipokea mapema hii leo 6 Machi katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Timu ya Taifa ya Uaandaaji wa Mkataba wa UNESCO 2005 akifafanua jambo kwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) Wakati wa kukabidhi taarifa ya utekelezaji wa mkataba huo mapema hii leo 6 Machi katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.
Picha na WHUSM – Dar es Salaam
6 Machi 2020

No comments :

Post a Comment