Thursday, March 5, 2020

SIMBACHAWENE AKUTANA NA WAJUMBE WA BODI YA SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA POLISI, JIJINI DAR ES SALAAM



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati), akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi, Prof. Suffian Bukurura, wakati alipokuwa anatoa taarifa ya Bodi hiyo, katika Kikao kilichofanyika Ukumbi wa Polisi, jijini Dar es Salaam, leo. Kulia ni Mwakilishi wa Inspekta Jenerali wa Polisi katika kikao hicho, ambaye pia ni Kamishna wa Ushirikishwaji wa Jamii, Dkt. Mussa Ali Mussa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati meza kuu), akimsikiliza Mjumbe wa Bodi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi, Hilda Tegwa, wakati alipokuwa anazungumza katika kikao cha Bodi hiyo, kilichofanyika Ukumbi wa Polisi, jijini Dar es Salaam, leo. Kulia ni Mwakilishi wa Inspekta Jenerali wa Polisi katika kikao hicho, ambaye pia ni Kamishna wa Ushirikishwaji wa Jamii, Dkt. Mussa Ali Mussa. Watatu kulia ni  Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Prof. Suffian Bukurura
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati), akimsikiliza Mwakilishi wa Inspekta Jenerali wa Polisi, ambaye pia ni Kamishna wa Ushirikishwaji wa Jamii, Dkt. Mussa Ali Mussa, wakati alipokuwa anazungumza katika kikao cha Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi kilichofanyika Ukumbi wa Polisi, jijini Dar es Salaam, leo. Kushoto meza kuu ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Prof. Suffian Bukurura.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), akisalimiana na Kamishna wa Jeshi la Polisi-Ushirikishwaji wa Jamii, Dkt. Mussa Ali Mussa, wakati alipokuwa anawasili jijini Dar es Salaam, leo, kwa ajili ya kukutana na Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi hilo, kilichofanyika Ukumbi wa Polisi, jijini Dar es Salaam, leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), akisalimiana na Katibu wa Bodi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi, John Massawe, wakati alipokuwa anawasili Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya Polisi, jijini Dar es Salaam, leo, kwa ajili ya kukutana na Wajumbe wa Bodi hiyo katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Polisi, jijini Dar es Salaam, leo. Kushoto ni Kamishna wa Jeshi la Polisi-Ushirikishwaji wa Jamii, Dkt. Mussa Ali Mussa. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments :

Post a Comment