Muonekano wa moja ya Eneo la kujisomea katika Maktaba mpya ya Chuo cha Ualimu Korogwe.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa akipata maelezo toka kwa mtaalamu
wa Tehama wa Chuo cha Ualimu Korogwe baada ya kuzindua Makataba ya Chuo
hicho
Chumba cha kompyuta katika Maktaba mpya ya Chuo cha Ualimu Korogwe
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania akikata Utepe kuashiria uzinduzi wa Maktaba mpya ya Chuo
cha Ualimu Korogwe, Tanga kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh Martin
Shigela, Mbunge wa Korogwe Mjini Mhe. Mary Chatanda na Kushoto ni Katibu
Mkuu Wizara ya Elimu , Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo
…………………………………………………………………………………………………………
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa Machi 5, 2020 amezindua
maktaba mpya ya Chuo cha Ualimu Korogwe kilichopo Mkoani Tanga.
Akizungumza na baadhi ya walimu
tarajali na wanafunzi aliowakuta katika maktaba hiyo
mara baada ya
kuizindua Waziri Mkuu amewataka wanafunzi hao kuitumia vyema maktaba
hiyo kwa lengo la kujipatia maarifa na kuongeza uwezo katika taaluma.
Naye Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akimkaribisha Waziri Mkuu amesema
Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 338 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maktaba hiyo ambayo ujenzi wake ukianza kwa Micjango ya Wananchi wa Korogwe.
Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 338 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maktaba hiyo ambayo ujenzi wake ukianza kwa Micjango ya Wananchi wa Korogwe.
Katibu Mkuu huyo amesema Serikali
ya Awamu ya Tano iliamua kutoa kiasi hicho cha fedha ili kuunga mkono
juhudi za wananchi ambao walichanga shilingi milioni 1.9 kwa ajili ya
kuanza ujenzi huo.
“Wananchi wa Korogwe waliona
umuhimu wa chuo hiki kuwa na maktaba na wakaanza kuchanga fedha na
kuanza ujenzi” amesema Dkt. Akwilapo.
Mmoja wa walimu tarajali katika
Chuo cha Ualimu Korogwe Emanuela Bombo ameishukuru Serikali kwa kuwekeza
kwenye ujenzi wa maktaba hiyo kwani itasaidia katika ujifunzaji.
Maktaba hiyo ina vifaa vya kisasa
pamoja zikiwemo kompyuta ambazo zinawezesha matumizi maktaba mtandao na
kwamba Maktana itatumiwa na walimu tarajali zaidi ya 1000 ambao wanasoma
masomo ya Sayansi, Hisabati na TEHAMA na pia wanafunzi wa shule za
Msingi na Sekondari wa wilaya ya Korogwe.
No comments :
Post a Comment