Bw. Ganga Ben Mlipano Meneja
Msaidizi Dawati la Malalamiko ya Wateja na Mabenki na Taasisi za Fedha
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) akitoa mada kuhusu Dawati hilo na namna
linavyofanya kazi katika semina ya waandishi wa habari kutoka vyombo
mbalimbali vya habari inayofanyika kwenye tawi la BoT jijini Arusha.
Baadhi ya waaandishi wa habari
wakimsikiliza Bw. Ganga Ben Mlipano Meneja Msaidizi Dawati la Malalamiko
ya Wateja na Mabenki na Taasisi za Fedha Benki Kuu ya Tanzania (BoT)
wakati akitoa mada kuhusu Dawati hilo na namna linavyofanya kazi katika
semina hiyo.
………………………………………………
Kuanzishwa kwa kanuni mpya za kusaidia kutatua malalamiko ya mteja (Bank Of Tanzania Financial Consumer Protection
Regulation) za mwaka 2019 kumesaidia kupunguza muda wa
malalamiko
mengi na ukomo wa kiwango kilichokuwa kimewekwa kwa wateja ambacho
kilikuwa ni shilingi milioni 15.000.000 lakini kwa sasa ni zaidi ya
fedha hizo.
Wateja wengi kwenye mabenki
walikutana na mikataba yenye lugha ngumu ambayo iliwachanganya na wengi
walichukua mikopo bila kujua faida na athari za mikopo hiyo jambo ambalo
liliwaletea usumbufu mwingi.
Bw. Ganga Ben Mlipano Meneja
Msaidizi Dawati la Malalamiko ya Wateja na Mabenki na Taasisi za Fedha
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ameyasema hayo wakati akizungumza na
waandishi wa habari mara baada ya kutoa kutoa mada kuhusu Dawati hilo
katika semina ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya
habari inayofanyika kwenye tawi la BoT jijini Arusha .
Bw. Ganga amesema ilikuwa
inachukua muda mrefu sana kuwarudishia wateja hati zao za dhamana ya
mkopo wakati wanapokuwa wamemaliza kulipa mikopo yao walikuwa
wamechukua.
Ameongeza kuwa malalamiko mengi
yalikuwa yakichukua muda mrefu kutatuliwa tofauti na sasa ambapo muda
huo umepungua sana ,Kwa mujibu wa kanuni hizo zimeweka muda mfupi zaidi
wa kutatuliwa kwa malalamiko ambao ni masaa sita, Masaa nane , Wiki moja
,Wiki Mbili na mengine ambayo ni magumu yatachukua siku 45.
Ameongeza kuwa kanuni hizi zina
ainisha kuwa benki inatakiwa kumweleza wazi mteja kwanini amenyimwa
mkopo, Mteja akishamaliza mkopo wake lazima arudishiwe hati yake
aliyoiweka kama dhamana haraka na kuhakikisha kwamba kama mteja
amenyimwa mkopo lazima aambiwe ndani ya siku saba.
Benki pia inatakiwa kumweleza
wazi mteja kuhusu mkopo anaochukua na athari zake ili kumuondolea
usumbufu wa kurudi benki mara nyingi akifuatilia mkopo wake na kujua
kama atapewa au hatapewa ikiwa ni pamoja na kujua faida na athari za
mkopo huo wakati atakapokuwa amechukua.
Amesema Sekta ya kibenki ni
muhumi sana kwa uchumi hivyo lengo la BoT ni kuhakikisha wateja
wanahudumiwa vizuri na kwa haraka ili waendelee kuweka fedha zao benki
badala ya kuweka nyumbani ili wakirudi nyumbani wawaambie na wengine
kuhusu umuhimu wa kuweka fedha zao benki na ubora wa huduma zinazotolewa
.
Benki Kuu ya Tanzania ilianzisha
Dawati la Malalamiko kwa ajili ya kutatua migogoro ya wateja Aprili mosi
mwaka 2015 na kutoka wakati huo mpaka sasa limetatua migogoro mingi
jambo ambalo limesaidia kupunguza matatizo kuhusu huduma za mabenki kwa
wateja wake.
No comments :
Post a Comment