Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini Suleiman Mzee akifanya mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na
Usalama, Jenerali Venance Mabeyo alipotembelea leo Makao Makuu ya Jeshi
ikiwa ni ziara yake maalum ya kujitambulisha kwa Wakuu wa Vyombo vya
Ulinzi na Usalama tangu aapishwe kuwa Mkuu wa Jeshi la Magereza Tanzania
Bara, Februari 3, 2020
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Seleman Mzee akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa, Diwani
Athumani alipomtembelea ofisini kwake leo mara baada ya mazungumzo.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Suleiman Mzee akisalimiana na Maafisa wa Uhamiaji alipowasili katika
Ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji, Jijini Dar es Salaam leo.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Suleiman Mzee (kulia) akiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,
Dkt. Anna Makakala (meza kuu) pamoja na baadhi ya Maafisa Waandamizi wa
Uhamiaji(hawapo pichani) alipotembelea Makao Makuu ya Uhamiaji, leo
jijini Dar es salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Brigedia Jenerali John
Mbungo (kushoto) akimkabidhi Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman
Mzee baadhi ya vipeperushi mbalimbali vyenye ujumbe wa mapambano dhidi
ya rushwa alipotembelea Ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam(Picha
zote na Jeshi la Magereza).
No comments :
Post a Comment