Friday, January 10, 2020

Wananchi wa mkoa wa Arusha wamshukuru Rais Magufuli kuwaongezea muda.


Wananchi wa jiji la Arusha wakiwa wamepanga foleni kwa ajili ya kupata Namba ya Nida  ili kuweza kusajili laini zao za simu ,kufuatia zoezi la pamoja la usajili Wa namba za simu kwa alama za vidole ambalo limeratibiwa na Mkuu Wa mkoa Mara kufuatia agizo la mh Raid John Magufuli kusogeza mbele zoezi la kusajili namba za simu kwa alama za vidole (picha na Happy Lazaro Arusha.
*******************************
Happy Lazaro,Arusha.
Wananchi wa mkoa wa Arusha wamemshukuru Rais John Magufuli kitendo cha kuwaongezea muda wa kusajili  laini zao za simu kwani asilimia kubwa ya wananchi bado hawajasajili laini.
Wakiongea wakati zoezi la kujiandikisha na kusajili namba zao za Nida linaloendelea katika viwanja vya kumbukumbu ya sheikh Amri Abeid walisema kuwa asilimia kubwa ya wananchi hawajasajili laini zao kwa alama za vidole kutokana na kutokuwa  na namba za Nida .
“Foleni hii kubwa sio kusajili kwa alama za vidole apana foleni hii imetokana na wananchi wengi hatuna namba za Nida ,kama Mimi nimejiandikisha tangu mwaka Jana zoezi lilivyoanza lakini hadi Leo sijapata namba wala kitambulisho nimekuja mara kibao mara niambiwe sionekani kwenye taarifa zao za Nida ,muda mwingine unakuta picha lakini huoni namba ” alisema Steven John
Walitumia muda huo kuomba Nida  kuongeza wafanyakazi pamoja na vitendea Kazi ili zoezi liweze kwenda  kwa haraka huku wakiwasisitiza kufungua mapema vituo vyao vya kuangalia namba za vitambulisho pamoja na  kujisajili .
“Leo wengine tumekuja saa  kumi na moja usiku ,wengine Saa moja tumekaa hapa Nida wamekuja kufungua saa tatu jamani kweli tunaomba wawahi basi kufungua ili watu waweze kufungua haraka na kiurahisi maana watu ni wengi sana na ikiwezekana muda wa kazi uongezwe tunaomba ili tupate huduma”Gloria Oktavina.
Akiongea na wananchi hao katika zoezi hilo, Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amewapongeza wananchi kwa namna ambavyo wamejitokeza kujiandikisha na kusajili namba zao kwa uvumilivu  , alisema kuwa serikali imejipanga vyema kuhakikisha  zoezi hili linaenda vyema kwa usawa .
“Viongozi wote wa halmashauri zote za mkoa wa Arusha watasimama imara kuhakikisha zoezi hili limekamilika ,tumegundua wananchi wengi walijiandikisha na hawajapata vitambulisho wala namba ila wanahakikisha watafanya Kazi usiku na mchana wanapata namba na zoezi limeisha salama” amesema Gambo.
Amesema katika kuhakikisha Zoezi linaenda linaisha haraka wataongeza eafanyakazi Wa Nida ambapo alisema watatumia vijana Wa JKT ili kuweza kukamilisha zoezi hili.
Naye meneja wa mawasiliano Kanda ya kaskazini (TCRA)Mhandisi Imelda Salim amesema kuwa,   kufuatia zoezi la pamoja la usajili wa namba za simu kwa alama za vidole ambalo limeratibiwa na Mkuu wa mkoa  kufuatia agizo la Rais John Magufuli kusogeza mbele zoezi la kusajili namba za simu kwa alama za vidole waliamua kusogeza kwa ukaribu zaidi huduma hii.
Amesema kuwa, wao kama TCRA kwa kushirikiana na taasisi zingine za Nida pamoja na makampuni ya simu wamekubaliana kushirikiana  ili kukamilisha maelekezo  yaliyotolewa na Rais  ,ambapo amesema kuwa zoezi hili limeanza katika halmashauri ya jiji la Arusha na wataendeleza katika halmashauri zote ili kila mwananchi ambae ajajiandikisha waweze kujiandikisha na kusajili namba yake ya simu.
Amebainisha kuwa, kuna changamoto ambayo imejitokeza  kwa wananchi wengine wakienda kujisajili laini zao kwa alama za vidole    wanakuta vidole vyao havimechi sasa tumetoa maagizo  iwapo mwananchi wakienda tatizo hili likimkuta aache taarifa zake apo na namba ya simu mtoa huduma atapeleka hizo taarifa Nida na zitafanyiwa Kazi na tutampigia kumpa mrejesho.

No comments :

Post a Comment