Monday, January 13, 2020

MADAKTARI WATATU MBALONI KWA TUHUMA ZA RUSHWA KAGERA.




********************************
Na Silvia Mchuruza.
Bukoba,Kagera.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoa wa Kagera inawashikilia watumishi wawili madaktari  na mmoja wao akiwa ni daktari wa kujisomea yaani PHD kwa
kile kilichodaiwa kuwa ni kujihusisha na vitendo vya rushwa na matumizi mabaya ya ofisi za umma.
Akizungumza na waandishi Wa habari katika ofisi za TAKUKURU mkoa Mkuu Wa TAKUKURU Ndg.John K.E Joseph amesema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa katika nyakati tofauti na kupitia wilaya tofauti za mkoa Wa kagera ambapo amewataj majina yao madaktari hao 
  “Ndugu wanahabari nichukue nafasi hii kutoa taarifa ya utendaji kazi Wa taasisi ya takukuru  toka Julai mosi mwaka 2019 hadi January 2020 ambapo tumefanya kazi nyingi sana lakini tumebahatika kuwatia mbaloni watumishi watatu ambapo wawili in madaktari Wa binadamu akiwemo Dr.Gresmus Gregery Nkrunzinza ambae ni mganga Mkuu Wa hospital teule ya wilaya ya biharamulo ambapo ameshitakiwa kwa kosa LA uchepushaji Wa dawa za mradi Wa akina mama wajawazito na wanaojifungua kwa kuziamisha na kupeleka kwenye duka binafsi la dawa na kuziuza pamoja”alisema  Mkuu Wa takukuru 
Aidha ameongeza kuwa daktari mwingine ambae pia nae ni daktari wa binadamu Dr.Gervas Dramas Maneto ambae anashikiliwa kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi na wizi akiwa mtumishi Wa ummba ambapo nae ni mwajiriliwa katika hospitality teule ya wilaya ya biharamulo.
” Daktari huyu kwa kutambua yeye ni mtumishi Wa umma na mwajiliwa Wa serikali  toka mwaka 2006  lakini mwaka 2011 alidiliki kuomba ajira nyingine  katika halmashauri ya ya jiji la mwanza na akapangiwa katika kiruo cha hospital ya Butihama na akawa analipwa mshahara mpaka mwaka 2014 January  jambo ambalo ni kinyume cha sheria” alisema Ndg.John K.E. Joseph.
Sambamba na hayo Mkuu Wa takukuru mkoa Wa kagera amesema kuwa katika kipindi hiki imemfikisha mahakamani Prof. Philemon Nyangi Wambura kwa makosa ya kuomba na kupokea rushes kutoka kwa wateja akiokuwa akiwashughulikia kikazi wakati  akiwa kaimu Mkuu Wa kampuni ya Ranchi za taiga  (NARCO).

No comments :

Post a Comment