Friday, January 10, 2020

FEZA BOYS YAJIVUNIA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE



Mwanafunzi wa shule ya sekondari ya wavula FEZA  Bw.Mvano Cabangoh akiwa pembeni na mama yake akiongea na wanahabari baada ya matokeo ya kidato cha nne kutangazwa wakati yeye akifanikiwa kushika nafasi ya sita kitaifa.
Mwanafunzi wa shule ya sekondari ya FEZA BOYS Bw.Mvano Cabangoh(aliebebwa juu) akishangiliwa na baadhi ya wanafunzi wenzake wa FEZA BOYS baada ya kutangazwa matokeo ya kidato cha nne wakati kwa upande wake akishika nafasi ya sita kitaifa.

Mkuu wa shule za FEZA nchini Bw.Ibrahim Yunus akiongea na wanahabari Jijini Dar es Salaam, baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kidato cha nne nchini wakati shule ya FEZA BOYS ikishika nafasi ya tatu Kitaifa.
*********************************
NA EMMANUEL MBATILO
Uongozi wa shule za FEZA hapa nchini umefurahishwa na matokeo yaliyotoka hasa baada ya
kufanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne.
FEZA Boys imefanikiwa kushika nafasi ya tatu kitaifa katika matokeo ya kidato cha nne wakati kwa upande wa wanafunzi shule hiyo imetoa mwanafunzi mmoja ambaye ameshika nafasi ya sita kitaifa.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, Mkuu wa shule za FEZA nchini Bw.Ibrahim Yunus amesema kuwa jitihada za pamoja ambazo zilikuwa zinafanywa na walimu, wanafunzi pamoja na wazazi ndizo chanzo cha shule hiyo kufanya vizuri kwenye matokeo ya mitihani ya kitaifa.
“Lengo la shule za FEZA kuweza kutoa elimu iliyobora kwa watanzania hasahasa tunazingatia tunakoelekea katika uchumi wa viwanda hivyo masomo ya sayansi tunayapa kipaumbele ili yaje yatujengee taifa letu”. Amesema Bw.Yunus.
Aidha, Bw.Yunus ametoa shukrani kwa wadau wote ambao wamewezesha elimu inayotolewa na shule hizo kuwa bora.
Kwa upande wa mwanafunzi ambaye amefanikiwa kushika nafasi ya sita kitaifa Bw.Mvano Cabangoh amesema kuwa siri ya kufanya vizuri katika mitihani yake ni pamoja na juhudi ambazo alikuwa anazifanya hasa kupangilia ratiba zisizombana kujisomea na muda wa kupumzika na kufanya mambo mengine pamoja na juhudi za wazazi na walimu katika ufundishaji.
“Sikutegemea kama naweza kushika nafasi hii ambayo nimepata maana kuingia katika kumi bora si rahisi kuna wanafunzi wengi nchi nzima hivyo ilikuwa ni ngumu sana kuingia kumi bora”.Amesema Bw.Cabangoh.

No comments :

Post a Comment