
Na.WAMJW-mwanza
Mpaka kufikia mwezi Septemba 2019
takribani watu 1,252,205 kati ya wananchi 1,600,000 wanaokadiriwa kuishi
na VVU nchini walikuwa wamepima na kufahamu hali zao za
maambukizi ya
VVU.
Hayo yamesemwa leo na Waziri wa
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakati wa maadhimisho
ya kitaifa ya siku ya UKIMWI duniani kitaifa yaliyofanyika jijini hapa.
“Hii ni sawa na asilimia 78.3 ya lengo la 90 ya kwanza.
Miongoni mwao wanaume walikuwa 413,985 sawa na asilimia 33, na wanawake walikuwa 838,220 sawa na asilimia 77″.
Miongoni mwao wanaume walikuwa 413,985 sawa na asilimia 33, na wanawake walikuwa 838,220 sawa na asilimia 77″.
Kwa upande wa vijana Waziri Ummy
amesema kuwa Vijana balehe (umri wa miaka 10 – 19) walikuwa 57,167 sawa
na asilimia 4.6, na vijana (umri wa miaka 15 – 24) walikuwa 96,006 sawa
na asilimia 7.7.
Aidha, amesema kati ya waliopima na kutambua afya zao watu 1,221,799 sawa na asilimia 97.6 wanatumia ARV.
Hata hivyo alisema Lengo la 90 ya
pili ambalo ni asilimia ya kuwa watu waliopimwa na kugundulika kuwa wana
maambukizi ya VVU wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU (yaani
ARV’s), tayari tumefikia takriban asilimia 98 wanatumia zawa za
kupunguza makali ya VVU yaani ARV.
“Lengo la 90 ya tatu, ambalo ni
kuhakikisha kuwa asilimia 90 ya wanaotumia ARV’s wamefanikiwa kupunguza
wingi wa VVU mwilini Waziri huyo alisema wamefanya vizuri sana,”ni kuwa
tumekuwa tukifuatilia kwa karibu hali za watu wanaotumia dawa za
kupunguza makali ya VVU”.Alisema
Waziri Ummy alitaja mafanikio
mengine ya kujikinga dhidi ya maambukizi ni tohara kwa wanaume ambapo
kuanzia mwaka 2009 hadi Agosti 2019 jumla ya wanaume 4,456,511
wamefanyiwa tohara kupitia njia za mkoba na huduma katika vituo vya
huduma
Takwimu zinaonesha kwamba watu
953,973 sawa na asilimia 89 ya watu 1,072,650 waliopimwa wingi wa VVU
wamefanikiwa kupunguza wingi wa VVU mwilini jambo ambalo ni muhimu
katika kinga dhidi ya UKIMWI.Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni
“Jamii ni chachu ya mabadiliko,tuungane kupunguza maambukizi mapya ya
VVU”
No comments :
Post a Comment