Wednesday, September 4, 2019

NDEGE YA ATCL AINA YA AIRBUS A220-300 ILIYOKUWA IMEZUILIWA NCHINI AFRIKA KUSINI YAACHILIWA

Mahakama ya Gauteng ya nchini Afrika Kusini imeamuru ndege ya Shirika la ndege Tanzania (ATCL) aina ya Airbus A220-300 iachiliwe.
Akizungumza na waandishi wa  habari mahakamani hapo leo Septemba 4, 2019, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa  Dkt. Damas Ndumbaro amesema leo katika video inayoonekana mitandaoni kuwa "Mahakama imetoa maamuzi yake kwa kuiachilia ndege ya Tanzania iliyokuwa imekamatwa hapa na kwamba hoja zote zilizoletwa na mawakili wetu zimekubalika kwahiyo tumeshinda kesi hiyo na imeamriwa kuwa ndege hiyo inaweza kuondoka." Alisema Dkt. Ndumbaro katika mahojiano hayo yanayoonekana kwenye ukanda wa video.
Alisema, mahakama imesema kama kuna hoja yoyote ile ya Bw.Hermanus Steyn anaweza kwenda kuifungua Tanzania kwasababu alikuja huku akisema kwamba kuna maamuzi ya msuluhishi lakini maamuzi ya msuluhishi yameshabadsilishwa na hukumu ya mahakama kwa hiyo amri ya mahakama ya Tanzania inaweza kutekelezwa na mahakama za Tanzania sio mahakama za Afrika Kusini.
Hata hivyo Naibu Waziri ameshangazwa na hatua ya Bw. Steyn ya kufungua kesi nyingine kupinga hukumu hii kabla haijasomwa na tunashangaa Bw. Steyn alijuaje kwamba hukumu hii itatoka dhidi yake yeye mpaka anakata rufaa tena hata kabla ya hukumu yenyewe kusomwa maana amekata rufaa jana wakati hukumu imesomwa leo kwahiyo sisi tunashangaa, lakini tunaishukuru mahakama ya Afrika Kusini kwa uamuzi wake na tunawashukuru Watanzania wote ambao wameunga mkono juhudi zetu za kuianasua ndege hii.

No comments :

Post a Comment