Mkuu wa kitengo cha uhifadhi wa mabaki ya vyanzo vya mionzi, katika Tume ya Nguvu za Atomic (TAEC) Nchini, Bw. Mikidadi Swalehe, akizungumza na waandishi wa habari.
Baadhi
ya washiriki wa mkutano wa majadiliano ya namna ya kutatua changamoto
na namna ya kuhifadhi na kuboresha usalama wa mabaki ya vyanzo vya
mabaki ya mionzi wakifuatilia kilichokuwa kikijadiliwa jijni Arusha.
Baadhi
ya washiriki wa mkutano wa majadiliano ya namna ya kutatua changamoto
na namna ya kuhifadhi na kuboresha usalama wa mabaki ya vyanzo vya
mabaki ya mionzi wakifuatilia kilichokuwa kikijadiliwa jijni Arusha.
Mwakilishi wa Shirika la Nguvu za Atomiki, Duniani, Bw. David Bannet David Bannet akitoa salamu za shirika hilo ambalo ni mwangalizi wa Kimataifa wa masuala ya matumizi ya teknolojia ya nyuklia
Baadhi
ya washiriki wa mkutano wa majadiliano ya namna ya kutatua changamoto
na namna ya kuhifadhi na kuboresha usalama wa mabaki ya vyanzo vya
mabaki ya mionzi wakifuatilia kilichokuwa kikijadiliwa jijni Arusha.
Baadhi
ya washiriki wa mkutano wa majadiliano ya namna ya kutatua changamoto
na namna ya kuhifadhi na kuboresha usalama wa mabaki ya vyanzo vya
mabaki ya mionzi wakifuatilia kilichokuwa kikijadiliwa jijni Arusha.
Baadhi
ya washiriki wa mkutano wa majadiliano ya namna ya kutatua changamoto
na namna ya kuhifadhi na kuboresha usalama wa mabaki ya vyanzo vya
mabaki ya mionzi wakifuatilia kilichokuwa kikijadiliwa jijni Arusha.

Na Vero Ignatus,Arusha.
Mkutano wa
Kimataifa wa siku tano kujadili mikakati mbalimbali ya kuboresha usalama katika
kuhifadhi mabaki ya vyanzo vya mionzi, unaendelea Jijini Arusha.
Mkutano
huo unakutanisha wataalam wa teknolojia ya nyuklia kutoka sehemu
mbalimbali duniani ili kujadili changamoto za usalama wakati
wa uhifadhi wa mabaki hayo, kwa nia ya kuepusha madhara kwa binadamu na mazingira
Mkuu wa kitengo cha uhifadhi wa
mabaki ya vyanzo vya mionzi, katika Tume ya Nguvu za Atomic (TAEC), Bw. Mikidadi Swalehe amesema mkutano huo unahudhuriwa na wanachama 30, kutoka nchi 21 duniani, ambapo umelenga
katika kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti vyanzo vilivyomaliza muda wake
lakini bado vinatoa mionzi.
Bw. Mikidadi alisema jukumu la kusimamia usalama linahitaji nchi
zote duniani, kuhakikisha kwamba, vyanzo vyote vya mionzi vinakuwa katika
mikono salama, ili kuepuka madhara mbalimbali ikiwemo kutumika kwa vyanzo hivyo
katika masuala ya ugaidi.
Alisema vyanzo vya mionzi vilivyomaliza matumizi vinahitajika kuhifadhiwa mahali
salama palipo na ulinzi maalum, kwani
hali hiyo itasaidia kuepusha vyanzo hivyo kuzagaa na kusababisha madhara
mbalimbali kwa binadamu na mazingira.
"Sisi kama TAEC tunalo jengo maalumu kwaajili
ya kuhifadhia vifaa hivyo vilivyomaliza matumizi yake." Alibainisha Bw. Mikidadi.
Kwa upande
wake Mwakilishi wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani (IAEA) Bw. David Bannet akitoa
salamu za shirika hilo ambalo ni mwangalizi
wa Kimataifa wa masuala ya matumizi ya teknolojia ya Nyuklia,a
liishukuru Tanzania hususani TAEC kukubali kuwa mwenyeji wa mkutano huo.
Aidha amesisitiza
kuwa IAEA itaendelea kushirikiana na nchi wanachama
kuhakikisha kuwa teknolojia ya nyuklia inatumika kwa matumizi salama ili isiathiri binadamu wa vizazi vilivyopo
sasa na vijavyo.
Awali mkutano
huo wa siku tano ulifunguliwa na Mkurugenzi mkuu wa TAEC Nhini Profesa Lazaro Busagala ambapo unatarajiwa
kumalizika leo.







No comments :
Post a Comment