Wednesday, September 4, 2019

mawakili 2000 wapatiwa elimu arusha



***********
Na Queen Lema, Arusha
zaidi ya mawakili 2000 kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini wanatarajiwa kupatiwa elimu juu masuala mbalimbali yahusuyo kazi zao na jamii kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha kazi
zao kwenye umma unaowazunguka
aidha mawakili hao wanatokea maeneo mbalimbali na watapewa elimu hiyo kwa kushirikiana na wanadau mbalimbali ambao wanawasilisha mada kwenye semina inayoendelea jijini arusha
akizungumza na fuulshangwe mapema leo afisa programu msaidizi kitengo cha mafunzo endelevu kwa mawakili kutoka chama cha mawakili (TLS)bi Rose Salvatory alisema mawakili hao watajifunza na kupatiwa mafunzo kwenye mada za muhimu ambazo ni nane
bi rose alifafanua kupitia mada hizo ambazo zitatolewa zitaweza kuwajengea uwezo wa namna ya kuendeleza taaluma yao lakini hata kuisaida serikali hususani kwa nyakati kama hizi za uchumi wa viwanda
‘kwa mfani unapoangalia katika mada hizi tuna mada juu ya makampuni ya biashara tunaaamini kuwa mtu kama wakili akiwa na anajua sheria hii ana uwezowa kumsaidia mtu mpaka kufikia hatua ya mwishi na baadae nchi ikapata mapato kwa hiyo ndio vitu vya msingi ambavyo tunaviangalia”aliongeza

No comments :

Post a Comment