Thursday, August 1, 2019

JPM APIGA PUSHAP 9 ZA NGUMI AKIZINDUA JENGO LA TATU LA ABIRIA (TBIII) LA KIWANJA CHA NDEGE CHA JULIUS NYERERE

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga Push Up na wasanii wa Tanzania One Theatre (TOT) wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakifunua pazia kama ishara ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakifurahia baada ya kuingia kwenye ndege ya ATCL aina ya Dreamliner iliyotua kutokea Mumbai wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijiandaa kuwapiga picha wapiga picha wa vyombo mbalimbali vya habari wakiwa ndani ya ndege ye ATCL ya Dreamliner iliyotua kutoka Mumbai wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019 



 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza kwa kazi nzuri ya kutumbuiza msanii wa Tanzania One Theatre (TOT) Plus Khadija Omar Kopa wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungia wananchi kwa furaha akiwa na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry bin  Ally na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki la Dar es salaam Muadhama Polycarp Kardinali Pengo wakati wakielekea kukata utepe wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere
jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019
Wapiga picha wakifurahia kupigwa picha na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ndani ya ndege ya Dreamliner ya AITCL iliyowasili kutoka Mumbai  wakati wa sherehe ya ufunguzi rasmi   wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Alhamisi Agosti 1, 2019x c c c

No comments :

Post a Comment