Thursday, July 11, 2019

WAZIRI WA SMZ, MHE. MAHMOUD THABIT KOMBO ATAMANI UTAALAMU WA BODI YA NAFAKA NA MAZAO MCHANGANYIKO TANZANIA(CPB) KUSHIRIKIANA NA TAASISI ZA ZANZIBAR KATIKA UFUNGASHAJI MAZAO

Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, (kulia), akiwa amebeba pakiti ya korosho huku akipatiwa maelezo na Afisa Masoko Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko, Bw. Peter Mobe ya namna ya kuandaa korosjo hizo tayari kwa mauzo toka kwa wakati alipotembelea banda la Bodi ya Nafaka na Mazao Machanganyiko kwenye maonesho ya 43 ya biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam, Julai 11, 2019.






NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, amefurahishwa na kazi zinazofanywa na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania (CPB) hususan namna ya ufungashaji wa korosho.
Mhe. Kombo ametembelea banda hilo leo Julai 11, 2019 ambapo alipata maelezo ya shughuli za bodi hiyo kutoka kwa Afisa Masoko, Bw. Peter Mobe ambaye alisema Bodi inafanya kazi ya kungeza thamani ya mazao kabla ya kuyapeleka sokoni.
“Tunanunua mazao kutoka kwa wakulima, na kisha tunaongeza thamani ya mazao hayo kabla ya kupeleka kwenye soko ndani na nje ya nchi” Alisema Bw. Mobe.
Alisema Bodi ya Nafaka na Mazao Machanganyiko ni Taasisi ya Serikali  iliyoanzishwa mwaka 2009 kwa Sheria namba 19 ikiwa na lengo la kufanya biashara ya Mazao ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko.
“Kwa sasa tunazo bidhaa za Unga wa dona unaitwa Dona Bora au chama nguvu, pia tuna Korosho ambayo tumeipa jina Korosho ya Tanzania au TanKorosho.” Alibainisha Bw. Mobe.
Naye Waziri Kombo alisema amefurahishwa na namna bidhaa hizo zinavyofungashwa hususan korosho kwani ufungashaji huo unawezesha bidhaa kukaa kwa muda mrefu bila kuharibika na hivyo kuna umuhimu wa taasisi zinazoshughulika na ufungashaji mazao huko Zanzibar zikafanya ushirikiano wa kubadilishana ujuzi na uzoefu na Bodi hiyo ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania.

No comments :

Post a Comment