
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta
ya Uchukuzi) Mhandisi Atashasta Nditiye,
amesema Ujenzi wa Jengo la tatu la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA)
umekamilika, na Jengo linatarajiwa kuanza uendashaji mwanzoni mwa mwezi Agosti mwaka huu.
Pia amesema amefurahishwa kwa kukamilika kwa
jengo hilo ambapo ni la
kisasa na huduma zake zake ni nzuri.
Akizungumza mara baada ya Ziara ya kukagua Jengo hilo
, amesema katika idadi ya miruko ya ndege Barani Afrika JNIA inachukua
nafasi ya tano na nafasi ya sita kwa idadi ya abiria.
‘’ Nimefurahishwa kwa kukamilika kwa Ujenzi wa jengo la tatu
la abiria wa Kiwanja cha Ndege ambapo utakapoanza kuhudumia abiria
natarajia tutachukua nafasi nzuri zaidi Barani Afrika kwani ni Jengo la kisasa
na litatoa huduma nzuri,’’ alisema.
Nae Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere( JNIA), Paul
Rwegasha akitoa ufafanuzi wa Kiwanja hicho, alisema mara baada ya
kukamilika kwa jengo la tatu itakuwa jumla ya majengo matatu yanaweza kuhudumia abiria milioni nane kwa
mwaka.
Rwegesha alisema ujenzi wa jengo la kwanza lina uwezo
wa kuhudumia abiria 500,000 kwa mwaka na ujenzi wa jengo la pili abiria milioni 1.5
Alisema kukamilika kwa jengo hilo la tatu kutaongeza idadi
ya Ndege, abiria pamoja na Watalii baada ya kuwa na Miundombinu bora na
ya kisasa.
Vile vile alisema Ujenzi wa jengo la tatu ni kwa ajili ya abiria wa safari za
Kimataifa ambapo kwa sasa yako mashirika
23 na jengo la pili kwa ajili ya abiria wa safari za
ndani ya nchi huku
jengo la kwanza safari za ndani
pia. .
Alisema ujenzi wa jengo la tatu la abiria litakuwa na
uwezo wa kuhudumia abiria 2,800, kwa saa na maegesho ya magari mchanganyiko
yasiopungua 2,075 kwa wakati mmoja.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
nchini (TAA), Mhandisi Julius Ndyamukama, alisema kwasasa kuna katika maandalizi ya Wakuu wa Nchi na Serikali
watakaohudhuria mkutano wa 39 wa SADC ambapo maadalizi yameambatana na
ukarabati wa maboresho ya miundombinu na samani.
Ndyamukama, alisema wageni hao wanatarajia kuingia hapa
nchini Agosti mwaka huu ambapo watapata huduma bora zaidi
na yenye uhakika.
Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha
Julius Nyerere Bw, Paul Rwegasha ( mwenye koti kijivu) Akitoa maelezo ya jengo
la mizigo linalokarabatiwa kwa Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano
Sekta ya Uchukuzi Mhandisi Atashasta Nditiye wakati alipofanya ziara katika
Kiwanja hicho.
No comments :
Post a Comment