Wanachama
na wadau wa mfuko wa PSSSF kwa watumishi wa umma
wakielekezwa kuhusu hifadhi ya jamii kwa wote. (Na Mpigapicha Wetu).
Na Christian Gaya. Majira Ijumaa 19.Julai.2019
Hifadhi ya jamii ni mfumo wa
jamii ambao umekuwapo tangu mwanzo wa mwanadamu. Tangu enzi za kale, jamii zote
zimekuwa na taratibu mbali mbali za kuhakikisha ya kwamba kila mtu anakuwa na
uhakika wa kuishi maisha yake katika mazingira yoyote yanayoweza...
kumkwaza
kuishi kama vile majanga ya maradhi, ulemavu na ya uzee.
Hifadhi ya jamii ina maana ni aina ya hatua madhubuti au
shughuli zilizobuniwa za kuhakikisha kuwa wananchi wa jamii hiyo wanapata
mahitaji yao ya lazima na ya msingi na
wanapewa kinga ya hifadhi ya kutokana na majanga ili kuwawezesha kuwa na kiwango
cha maisha ya kuishi kulingana na mila na desturi za jamii.
Malengo ya hifadhi ya jamii ni kumwezesha
mwananchi kuishi maisha yenye staha kwa kuwawezesha kupata huduma za msingi
pale wanapokuwa hawana kipato kutokana na sababu mbalimbali zinatokana na uzee,
kifo, ugonjwa, uzazi na kadhalika
Wazee, watoto, yatima, wajane,
na wagonjwa ambao kutokana na hali zao hawawezi kujikimu ni baadhi ya makundi
ambayo yamekuwa yakipata kinga maalumu tangu enzi hizo hadi sasa, kama sehemu
ya mfumo wa jamii ya mwanadamu duniani kote.
Jamii ilikuwa inahakikisha
kuwa vikundi hivyo vya watu wasiojiweza wanapata hifadhi ya jamii kwa maana ya
msaada wa chakula, malazi na matibabu.
Ili kuweza kutoa hifadhi hiyo
jamii ilijiwekea taratibu na kanuni ambazo ilibidi zifuatwe kabla ya mtu
hajapewa hifadhi kwa nia ya kuhakikisha kuwa ni wale tu wanaohitaji msaada
ndiyo wanaopata. Na utaratibu mpaka leo unafanyika ndani ya jamii za Kitanzania
na penginepo pale hapa Afrika na hata Ulaya.
Hifadhi ya jamii ni haki ya
msingi ambayo kila mtu anastahili kupata kutoka katika jamii. Jamii zilijiwekea
utaratibu na sheria ambazo hutumika kuhakikisha jamii inapoondokana na
utegemezi.
Sheria ya kwanza kabisa
kutungwa na kuandikwa kuhusu hifadhi ya jamii ilikuwa in ile sheria ya kusaidia
maskini huko uingereza iliyotungwa karne ya 16. Sheria hiyo ilifuatiwa na
nyingine iliyotungwa mwaka 1883 kwa ajili ya matibabu.
Baadaye nchi nyingi hasa za
ulaya zilianza kutunga sheria mbalimbali kwa ajili ya kuanzisha mifumo ya
hifadhi ya jamii. Na hiyo ilitokana na mapinduzi ya viwanda yaliyo tokea ulaya
wakati huo, ambapo watu wengi walikimbilia mijini kutoka mashambani kwa kazi ya
kuajiriwa viwandani.
Hivyo misingi ya kusaidiana
kifamilia kwa watu wa mashambani, kifamilia kwa watu wa mashambani ikaanza kupotea.
Kwa sababu nguvukazi yote iliyokuwa ukitoa huduma katika koo mbalimbali
iliishia kwenda mijini kwenda kufanya kazi.
Lakini ikumbukwe kuwa hifadhi
ya jamii ilitolewa na mpaka sasa bado inatolewa ndani ya jamii mbalimbali za
kiafrika ingawa kiwango chake kila siku kinakwenda kikipungua hasa kutokana na
mabadiliko ya kiuchumi na kijamii duniani.
Na ndiyo maana wazee wengi
wana imani hata ya kuzaa watoto wengi zaidi kama hifadhi yao ya jamii ya sasa
na ya baadaye ingawa lengo kubwa ni kuendeleza ukoo na kufanya kuwa ni wajibu
kuwa na watoto.
Watu wanateuliwa kubaki na
wazee na wale wengine wasiojiweza ili kuwapa hifadhi ya jamii. Hata wakunga wa
jadi tunao mpaka sasa ambao hutoa huduma za hifadhi ya jamii kwa akina mama
wajawazito na wanapojifungua.
Watoto waliofiwa na wazazi wao
wana ukoo waligawana na kuwapa hifadhi ya jamii mpaka wanapofikia umri wa
kujitegemewa na yule anayesoma anapewa hifadhi mpaka anapomaliza elimu ya juu. Huo
ni utaratibu ambao unawekwa na wanajamii hasa ndani ya koo mbalimbali. Na
tumeona aina hii ya hifadhi ya jamii inaendelea kufanyiwa kazi na baadhi ya
jamii.
Tumeona mara nyingi karibu
mikoa yote hapa nchini huduma ya kupatiwa msaada wa mazishi unapotolewa ndani
ya vikundi mbalimbali. Na watu sasa wamegundua kuwa njia nzuri ya hifadhi ya
jamii ni kwa ile isiyokuwa rasmi ambapo kuna vikundi mbalimbali vya kufa na
kuzikana, kuweka na kukopa, ambapo wanachama wake hutokana na mkoa au wilaya
anakotoka.
Na hata viongozi wakuu wa
mashirika ya umma, mashirika yasiyo ya kiserikari, na wa serikali wamekuwa
wanachama wachagiaji wakubwa kwenye mifuko hii isiyo rasmi.
Na hii imeleta changamoto
kubwa kwa hifadhi za jamii zilizo rasmi kama vile mashirika ya hifadhi ya jamii
yaliyopo hapa nchini na sehemu zingine za kiafrika.
Kwa kawaida anayetakiwa
kuwajibika kutoa hifadhi ya jamii kwa wazee, walemavu, wategemezi, na kwa watu
wasio na kazi ni serikali na jamii ya kitanzania kwa ujumla.
Hifadhi ya jamii ina maana ni
aina ya hatua madhubuti au mfuko uliobuniwa kama vile wa PSSSF wa kuhakikisha kuwa wananchi wa jamii hiyo
wanapata mahitaji yao ya lazima na ya msingi
na wanapewa kinga ya hifadhi ya kutokana na majanga ili kuwawezesha kuwa
na kiwango cha maisha ya kuishi kulingana na mila na desturi za jamii.
Serikali kupitia sheria ya
mfuko wa hifadhi ya jamii kwa watumishi wa umma namba 2 ya mwaka 2018 ilifuta
mifuko ya hifadhi ya jamii ya PPF, PSPF, LAPF, na GEPF na kuanzisha mfuko wa
hifadhi ya jamii kwa watumishi wote wa umma yaani PSSSF.
Inaendelea
wiki ijayo
No comments :
Post a Comment