Saturday, June 15, 2019

WAZIRI UMMY ATOA TAHADHARI KUHUSU EBOLA


Na WAMJW- Mwanza
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ametoa tahadhari kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Ebola ulioripotiwa katika nchi ya demomokrasia ya Kongo na sasa
katika nchi jirani ya Uganda.
Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati akitoa tamko kuhusu ugonjwa wa Ebola katika kituo kilichotengwa kwa ajili ya magonjwa ya mlipuko ikiwemo wahisiwa wa Ebola endapo utaingia nchini.
Waziri Ummy ametoa tahadhari kwa Mikoa yote ya Tanzania, kuchukua hatua stahiki za kujikinga na kudhibiti ugonjwa wa Ebola usiingie nchini kwa kutekeleza baadhi ya mambo ikiwemo, kuepuka kugusa damu, mkojo, jasho, kinyesi, machozi na majimaji mengine yanayotoka Mwilini mwa Mgonjwa mwenye dalili za ugonjwa wa, Ebola.
Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa Mkoa wa Mwanza ni moja kati ya mikoa mitatu iko katika hatari zaidi ya kupata Ugonjwa huo, ikifuatiwa mkoa wa Kagera,
Hata hivyo, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imekwishapeleka jumla ya seti 3,500 za vifaa kinga kwa ajili ya watumishi wa afya kupitia ofisi za kanda za MSD.
Aliendelea kusema kuwa, kutokana na tishio la sasa tutaongeza seti 4,000 na kuzipeleka karibu zaidi na wananchi ikiwa ni pamoja na kwenye hospitali zote za Mikoa na Wilaya kwa ajili ya kujiandaa.

No comments :

Post a Comment