Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA) Kanda ya Ziwa imeendesha mkutano wa wadau wa wa sekta ya
mawasiliano Kanda ya Ziwa kwa ajili ya kupokea maoni,mapendekezo na
kusikiliza kero zinazohusu utendaji wa TCRA.
Mkutano huo wa siku moja umefanyika leo
Juni 13,katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza na
kukutanisha wadau mbalimbali wakiwemo watoa maudhui kupitia
TV,Radio,mitandao,mafundi simu,polisi,wauzaji na wasambazaji wa vifaa
vya mawasiliano na wadau wengine.
Akizungumza wakati wa mkutano huo,Mkuu
wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo aliyataja baadhi ya
majukumu ya TCRA kuwa ni kuimarisha ustawi wa Watanzania kupitia ukuzaji
wa ushindani katika sekta ya mawasiliano wenye kuleta uchumi
fanisi,kulinda maslahi ya watumiaji wa taarifa mbalimbali za
mawasiliano.
Mhandisi Mihayo alisema jukumu jingine
ni kusimamia upatikanaji wa huduma zinazokidhi viwango na vigezo na
masharti ya usambazaji wa bidhaa na huduma za mawasiliano,kudhibiti tozo
na viwango vinavyohusiana na huduma za mawasiliano,kusimamia utendaji
kazi wa sekta ya mawasiliano ukilinganisha na kiwango cha utekelezaji
uliowekwa.
Katika hatua nyingine alisema hadi
kufikia Juni 10,2019 kumekuwepo na ongezeko kubwa katika eneo la simu za
viganjani,huduma za intaneti,vituo vya redio ambapo sasa kuna
makampuni sita yanayotoa huduma za simu na internet na makampuni manne
yanayotoa huduma za internet pekee.
“Pia tuna vituo 38 vya utangazaji wa
redio,vituo viwili vya utangazaji wa televisheni wanaorusha matangazo
yao kupitia MUX operators,makampuni 24 ya utangazaji wa televisheni kwa
kutumia teknolojia ya Cable na makampuni/taasisi 32 zinazotumia simu za
upepo na watoa huduma 373 wanaojihusisha na biashara ya
kuagiza,kusambaza na kuuza vifaa vya mawasiliano",alifafanua.
ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mkuu wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo akizungumza kwenye mkutano
wa wadau wa wa sekta ya mawasiliano Kanda ya Ziwa kwa ajili ya kupokea
maoni,mapendekezo na kusikiliza kero zinazohusu utendaji wa TCRA.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkuu wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo akifungua mkutano wa wadau wa wa sekta ya mawasiliano Kanda ya Ziwa.
Mkuu wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo akifungua mkutano wa wadau wa wa sekta ya mawasiliano Kanda ya Ziwa.
Wadau wa wa sekta ya mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini.
No comments :
Post a Comment