MWILI
wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kampala (KIU), kampasi ya Gongolamboto jijini
Dar es Salaam, Anifa Simpolianus C. Mgaya (22), umeagwa leo nyumbani kwao marehemu
Mbezi SalaSala, jijini Dar es Salaam ambapo Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani,
Mhandisi Yusuph Masauni na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro
Mambosasa walikuwa viongozi wa juu wa serikali waliohudhuria shughuli hiyo. Anifa
aliuawamajira ya usiku Juni 17, 2019
jirani kabisa na lango la kuingilia chuoni hapo na watu wanaosadikiwa kuwa
vibaka. Tayari Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limetangaza leo
Juni 19, 2019 kuwa limemkamata kijana wa miaka 19, Ernest Joseph kwa tuhuma za
mauaji hayo. Mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda mkoani Iringa kwa mazishi
Kamanda wa Polisi Kanda
Maalumu ya Dar es Salaam,Lazaro Mambosasa akizungumza wakati wa ibada ya kumuaga mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha
Kampala, Anifa Simpoliunus, aliyefariki baada ya kuvamiwa na vibaka maeneo
karibu na chuo hicho.Ibada hiyo imefanyika nyumbani kwa marehemu Mbezi
SalaSala,jijini Dar es Salaam. Mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda mkoani
Iringa kwa mazishi
Naibu Waziri wa Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akitoa heshima za mwisho
mbele ya jeneza lililobeba mwili wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha
Kampala, Anifa Simpoliunus, aliyefariki baada ya kuvamiwa na vibaka maeneo
karibu na chuo hicho.Ibada ya kuaga mwili imefanyika nyumbani kwa marehemu
Mbezi SalaSala,jijini Dar es Salaam. Mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda
mkoani Iringa kwa mazishi
Kamanda wa Polisi Kanda
Maalumu ya Dar es Salaam,Lazaro Mambosasa akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza
lililobeba mwili wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala, Anifa
Simpoliunus, aliyefariki baada ya kuvamiwa na vibaka maeneo karibu na chuo hicho.Ibada
ya kuaga mwili imefanyika nyumbani kwa marehemu Mbezi SalaSala,jijini Dar es
Salaam. Mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda mkoani Iringa kwa mazishi
Waombolezaji wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani)wakati wa ibada ya kuaga
mwili wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha
Kimataifa cha Kampala, Anifa Simpoliunus, aliyefariki baada ya kuvamiwa na
vibaka maeneo karibu na chuo hicho.Ibada hiyo imefanyika nyumbani kwa marehemu Mbezi
SalaSala,jijini Dar es Salaam. Mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda mkoani
Iringa kwa mazishi .(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
No comments :
Post a Comment