Mashirika ya habari
MZIMU wa
Uingereza kujitoa kwenye Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU), unaendelea kuitafuna
nchi hiyo ambapo leo Mei 24, 2019, Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Bibi.Theresa May (pichani) ametangaza...
kujiuzulu wadhifa huo.
Akiwa mbele ya
lango la ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza 10 Downing Street leo Mei 24, 2019,
Bibi May alisema,
“Nimejitahidi kuwashawishi
wabunge kuhakikisha suala la Brixit la (Mchakato wa Uingereza kujitoa EU),
kupitia Bunge linafikia mahala pazuri lakini imeshindikana kwa hivyo sina budi
kuachia madaraka ya uongozi wa chama cha Conservative ifikapo Juni 7, 2019.”
Alisema Bibi May kwa majonzi makubwa.
Alisema, “Ninaondoka
nikiwa Waziri Mkuu wa pili mwanamke, lakini haimaanishi nitakuwa wa mwisho, kwa
heshima kubwa nimejivunia kushika nafasi ya Waziri Mkuu.” Alisema.
Hata hivyo
atasalia kwenye nafasi hiyo hadi mwezi Julai atakapochaguliwa kiongozi mwingine
wa chama.
Theresa May
anakuwa waziri Mkuu wa pili wa nchi hiyo kujiuzulu wadhifa huo katika kipindi
hiki cha msukosuko wa nchi hiyo kujiondoa katika ushirika na Jumuiya ya Ulaya,
waziri Mkuu wa kwanza kukumbwa na wimbi hili alikuwa David Cameron.
Miaka miwili
iliyopita David Cameron alijiuzulu baada ya wananchi wa Uingereza kupiga kura
ya ndiyo ya kujiondoa kwenye Jumuiya ya Ulaya wakiushinda upande wa chama chale
cha Labour kilichokuwa kinapinga Uingereza kujitoa.
No comments :
Post a Comment