Monday, April 1, 2019

TAKUKURU DODOMA, YAOKOA MILIONI 152, HUKU MILIONI 900 ZIKICHUNGUZWA


DSC_2585
Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Dodoma Sosteneth Kibwengo akizungumza na wanahabari hawapo pichani, akitoa taarifa ya utendaji wa taasisi hiyo kwa robo ya mwaka.
……………………………
Na EZEKIEL MTONYOLE, DODOMA.
Taasisi ya Kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU, Mkoa wa Dodoma, imefanikiwa kuokoa zaidi ya shilingi milioni mia moja hamsini na mbili zilizokuwa zilipwe  kwa
wakandarasi ambao hawakutimiza majukumu yao kikamilifu katika miradi waliyopewa.
Pia jumla ya shilingi milioni mia tisa(9000,000,000) zinachunguzwa baada ya kuwa na viashiria vya rushwa katika miradi mbalimbali.
Hayo yamebainishwa leo mkoani hapa na kamanda wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU, mkoa wa Dodoma Sosteth kibwengo wakati akitoa taarifa ya robo ya mwaka kwa wanahabari.
Ambapo amesema kwa robo ya mwaka taasisi hiyo imefanikiwa kuokoa zaidi ya shilingi mia moja na hamsini na mbili(152), zilizokuwa zilipwe kwa wakandarasi ambao hawakutekeleza majukumu yao kikamilifu.
“Katika miradi iliyofuatiliwa, fedha Sh. milioni mia tisa (900,000,000) inachunguzwa baada ya viashiria vya jinai kuonekana, TAKUKURU pia imefanikiwa kuokoa kiasi cha Sh. milioni mia moja hamsini na mbili na laki tatu (152,300,000) ambazo zingelipwa kwa wakandarasi ambao ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi ya maji umebaini hawakutimiza majukumu yao ipasavyo” amesema Kibwengo.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa pia imemtaka mkurugenzi wa kampuni ya Global Space East Africa Limited, inayojenga kituo cha afya Mima kilichopo Wilayani Mpwapwa mkoani hapa kulipoti katika ofisi ya zake zilizopo wilayani humo kwa mahojiano.
“Pia tumebaini udanganyifu katika mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Mima wilayani Mpwapwa hivyo tunamtaka Mkurugenzi wa kampuni ya Global Space East Africa Limited ya Dare esaalam, bw. Gaston Meltus Francis ambaye kampuni yake ilipewa kazi hiyo kuripoti mara moja kwenye ofisi zetu za wilaya ya Mpwapwa” amesema.
Vile vile alibainisha kuwa katika kipindi husika, TAKUKURU ilipokea jumla ya taarifa tisini na sita (96) za rushwa na makosa yahusianayo ambapo sekta  ziliongoza kwa tuhuma mi.
Serikali za mitaa (25%), Ardhi (17%), Elimu (16%), Afya (8%), Maji, Ujenzi na Mahakama (kila moja asilimia 7), na Polisi (6%), taarifa hizo zilifanyiwa kazi kwa njia mbalimbali na majalada nane (8) ya uchunguzi yalikamilika ikiwa ni ongezeko la asilimia 12.5 ya majalada yaliyokamilika kwa kipindi hicho mwaka 2018.
Aidha tumefungua kesi mpya tano (5) na kesi nne (4) zilitolewa maamuzi na Mahakama ambapo Jamhuri imeshinda zote kwa washtakiwa kutiwa hatiani na kuhukumiwa vifungo mbalimbali.
Aidha alisema kwa robo ya Aprili hadi Juni, 2019, pamoja na majukumu mengine TAKUKURU inakusudia kuongeza juhudi katika ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya kimkakati mkoani Dodoma ikiwemo ya ujenzi wa barabara; kuchambua mifumo ya ukusanyaji wa kodi na mapato ya serikali; na kuendelea kuelimisha umma madhara ya rushwa katika uchaguzi.
Vile vile alibainisha kuwa TAKUKURU inawataka wajumbe wa Kamati za Ujenzi na Manunuzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo kuzingatia taratibu za matumizi ya fedha za serikali na kuwaasa wasikubali kurubuniwa na viongozi wasio waadilifu kwani wao ndio watakaowajibika.
Pia aliwataka watendaji kutoa nyaraka tunazohitaji kisheria kwa wakati ili waweze kutekeleza majukumu yao na kuwaasa wale wanaojaribu kukwamisha kwamba kitendo hicho ni kosa la jinai na hatua stahiki zitachukuliwa dhidi yao.

No comments :

Post a Comment