Tuesday, April 2, 2019

SPIKA NDUGAI MGENI RASMI UZINDUZI WA MATANGAZO YA IDHAA YA KISWAHILI BBC UDOM JIJINI DODOMA


V25A7820
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Prof. Donald Mpanduji alipoalikwa kama Mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC tukio lililofanyika tarehe 1 Aprili, 2019, Chuo Kikuu cha Dodoma Mjini Dodoma.
V25A7864A
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia mbele) akiongozana na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Prof. Donald Mpanduji (kushoto mbele) wakielekea ukumbini kwa ajili ya Uzinduzi wa Matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC tukio lililofanyika tarehe 1 Aprili, 2019, Chuo Kikuu cha Dodoma Mjini Dodoma . Spika Ndugai alialikwa kama Mgeni rasmi katika tukio hilo
V25A7896A
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akipatiwa maelezo na Afisa kutoka Idara ya Kiswahili Chuo Kikuu cha Dodoma, Ndg. Gervas Kasiga kuhusu huduma zinazotolewa na Idara hiyo ikiwa ni pamoja na Masuala ya Utafiti na Ushauri, kabla ya kuelekea Ukumbini kwa ajili ya kuzinduzi  Matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC tukio lililofanyika tarehe 1 Aprili, 2019, Chuo Kikuu cha Dodoma Mjini Dodoma. Spika Ndugai alialikwa kama Mgeni rasmi katika tukio hilo
V25A7916A
Wanafunzi na Wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma wakiwa katika uzinduzi wa Matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC tukio lililofanyika tarehe 1 Aprili, 2019, Chuo Kikuu cha Dodoma Mjini Dodoma. Katika tukio hilo Spika Ndugai alialikwa kama Mgeni rasmi
V25A7986A V25A7976A V25A7989A
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Wanafunzi, Wahadhiri na Wageni Mbali mbali wakati wa uzinduzi wa Matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC tukio lililofanyika tarehe 1 Aprili, 2019, Chuo Kikuu cha Dodoma Mjini Dodoma. Katika tukio hilo Spika Ndugai alialikwa kama Mgeni rasmi
V25A7932A
Kwaya ya Chuo Kikuu cha Dodoma wakiimba wakati wa uzinduzi wa Matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC tukio lililofanyika tarehe 1 Aprili, 2019, Chuoni hapo Mjini Dodoma. Katika tukio hilo Spika Ndugai alialikwa kama Mgeni rasmi
\V25A8045A
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Prof. Donald Mpanduji (wa tano kushoto), Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Ndg. Godwin Kunambi (wa pili kulia), Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe (wa tatu kushoto), Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Dodoma, Ndg. Aziza Mumba (kulia) na wageni Mbali mbali baada ya Uzinduzi wa Matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC tukio lililofanyika tarehe 1 Aprili, 2019, Chuo Kikuu cha Dodoma Mjini Dodoma. Katika tukio hilo Spika Ndugai alialikwa kama Mgeni rasmi
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments :

Post a Comment