Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa
Leila burhan Ngozi akizungumza na Vijana mbali mbali katika Tawi la CCM
Miti Ulaya lililopo Jimbo la Malindi.
VIJANA wa UVCCM wakiwa katika
matembezi ya Amsha amsha ya kuimarisha Chama Cha Mapinduzi katika Jimbo
la Malindi Zanzibar wakiongozwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa
Leila burhan Ngozi.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa
Leila burhan Ngozi akikabidhi Cheti kwa mshiriki wa Matembezi ya Siku
ya kumbukumbu ya Mashujaa mwaka 2019.
…………………………………………………………………………………..
NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha
Mapinduzi(CCM) Taifa Leila Burhan Ngozi amesema hakuna Chama cha Siasa
chochote kitakachozuia Ushindi wa CCM kwa ngazi zote
katika Jimbo la
Malindi katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Msimamo huo ameutoa leo katika
Matembezi ya kuimarisha uhai wa Chama ya ‘Amsha amsha’ yenye kauli mbiu
ya Malindi ya Kijani inawezekana ya kushusha Bendera kongwe na
kupandisha mpya katika Matawi,Maskani ,Ofisini na Majengo mbali mbali
yanayomilikiwa na CCM na Jumuiya zake katika Jimbo hilo.
Alisema mwaka 2020 ndio wakati
mwafaka wa kulikomboa Jimbo hilo likarudi mikononi mwa CCM hatua
itakayopelekea Wananchi wa eneo hilo kuendelea kunufaika na Matunda ya
Serikali za Chama Cha Mapinduzi.
Alisema CCM ina nafasi ya
Mwakilishi na Madiwani na Mbunge ni wa upinzani hali inayopelekea
kutokuwepo kwa ushirikiano katika Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwani
wapinzani wamekuwa wakikwamisha kwa makudi mipango ya maendeleo huku CCM
ikitoa Huduma kwa Jamii kupitia Mwakilishi wake.
Mjumbe huyo wa Kamati Kuu Leila,
alifafanua kwamba ridhaa ya kulitwaa Jimbo hilo kuwa la CCM itatoka kwa
Wananchi wenyewe ambao wameonyesha nia ya kuiamini CCM.
Katika maelezo yake Leila,
alieleza kwamba CCM tayari inajivunia Utekelezaji mzuri wa Ilani yake
katika maeneo mbali mbali Nchini likiwemo Jimbo la Malindi, hatua
inayotakiwa kupongezwa na kila mwananchi ambaye ni Mzalendo.
Alisema kasi ya CCM ya
kuwapelekea wananchi maendeleo endelevu itaendelea kuongezeka kila siku
zikienda kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, kwani Wananchi
wanataka maendeleo na sio maneno ya porojo na ahadi hewa.
Alizisisitiza Jumuiya zote za
Chama Cha Mapinduzi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kwa mujibu wa
kanuni na miongozo yao ili mwaka 2020 CCM ishinde kwa kishindo.
Pamoja na hayo aliupongeza
Uongozi wa UVCCM Wilaya ya Mjini kwa kuanzisha kampeni hiyo ya ‘Amsha
amsha’ katika Jimbo la Malindi inayoimarisha uhai wa Chama na Jumuiya
zake kwa ujumla.
Alisema changamoto zote
zilizotajwa katika risala za Matawi ya Vijana zinazotakiwa kutafutiwa
ufumbuzi wa haraka ataziwasilisha katika ngazi za Uongozi wa CCM ili
zitafutiwe ufumbuzi wa kudumu.
Aliwakumbusha Vijana kuchangamkia
fursa za Kielimu zilizopo nchini sambamba na kujiunga na Vituo mbali
mbali vya Mafunzo ya Amali ili wapate ujuzi na utaalamu wa kuwawezesha
kujiajili wenyewe.
“Serikali zetu zipo katika Safari
ya kutafsiri kwa vitendo Sera ya Uchumi wa Viwanda kwa kuaulisha
Viwanda Vidogo Vidogo na Vikubwa vifanye kazi ili wananchi wapate ajira
lakini pia tuzalishe bidhaa nyingi na kuuza nje ya Nchi kwa lengo la
kuingiza fedha za Kigeni.”,alisema Leila.
Aliwasihi Wanachama wa Chama Cha
Mapinduzi kila mmoja kwa nafasi yake kuhakikisha wanaongeza wanachama
wapya watakaopiga kura za ndio zitakazokipatia ushindi Chma mwaka 2020
na kiendelee kuongoza Dola.
Naye Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa
Mjini Kamaria Suleiman Nassor alisema matembezi hayo katika Jimbo hilo
wanajaribu mitambo ya kuelekea katika uringo wa Mapambano ya Kisiasa ya
mwaka 2020.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
UVCCM Wilaya ya Mjini Hudhaima Mbarouk Tahir, aliwashukru Vijana mbali
mbali wa UVCCM walioshiriki katika amsha amsha hiyo iliyohamasisha
Wanachama wa CCM na kutuma ujumbe mzito kwa wapinzani wa Jimbo la
Malindi.
Hudhaima alieleza kuwa matembezi
hayo yatakuwa endelevu katika Majimbo mbali mbali yaliyopo katika Wilaya
hiyo kwani ni sehemu ya kuwaunganisha Vijana na kuwajenga kuwa
wazalendo wa kukipenda Chama Cha Mapinduzi muda wote.
Kupitia matembezi hayo Mjumbe wa
Kamati Kuu ya CCM Taifa Leila Burhan Ngozi amewatunuku Vyeti Vijana
mbali mbali walioshiriki matembezi ya kuwaenzi Waasisi wa Mapinduzi ya
mwaka 2019,ametoa Kadi za Uanachama kwa Wanachama wapya wa UVCCM pamoja
na kupandisha Bendera katika Ofisi za Chama na Jumuiya pamoja na
kutembelea kikundi cha Ushirika.
No comments :
Post a Comment