Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt
Respicious Boniface akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya
kuwapokea wakufunzi wa kutoa dawa usingizi kutoka nchini Latvia katika
ukumbi mpya wa mikutano wa MOI
Dkt Iveta
Gobovska kutoka Chuo Kikuu cha Ltvia akizungumza jambo katika hafla
maalumu ya kupokelewa na kuanza kwa mafunzo ya kuwapatia wagonjwa dawa
za usingizi kwa njia ya kisasa (Regional block anaesthesia) hifla hiyo
imefanyika leo katika Taaisisi ya MOI
Katibu mkuu wa chama cha mabadkari
bingwa wa Usingizi Tanzania SATA Dkt Albert Ulimali akifafanua jambo
kwa waandishi wa habari. [NA Andrew Chale)
……………………….
NA ANDREW CHALE
TAASISI ya tiba ya Mifupa MOI
imeanzisha huduma ya kutoa dawa za usingizi (Reginal block Anaesthesia)
ambapo eneo husika linalofanyiwa upasuaji ndilo litakolo husika kwa
kuzuia mishipa ya fahamu na hivyo mgonjwa kuwa macho na kuzungumza au
hata kusoma gazeti
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi
Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface katika hafla ya kuwapokea
wakufunzi wawili kutoka Chuo kikuu cha Latvia cha nchini Latvia ambao
watatoa mafunzo hayo ya kibingwa ya kuzuia mishipa ya fahamu katika eneo
linalofanyiwa upasuaji badala ya kumlaza mgonjwa usingizi (Nusu kaputi)
kwa zaidi ya siku kumi kwa madaktari bingwa wa MOI na madaktari walio
mafunzoni
“Huu ni muendelezo wa mafunzo
ambayo tulishayaanzisha kwa mdakatari wetu , lengo kubwa la mafunzo haya
na ujio wa wakufunzi hawa ni kuhakikisha huduma hii inaendlea kutolewa
hapa MOI. Ni mbinu bora na salama ya kumlaza mgonjwa kwaajili ya
upasuaji ambapo mgonjwa anaweza kufanyiwa upasuaji huku anasoma kitabu
(Novel) ambapo baada ya upasuaji mgonjwa hapati maumivu makali na
anaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani siku hiyohiyo” Alisema Dkt Boniface
Dkt Boniface amesema pamoja na
wakufunzi hawa kutoa mafunzo , Taasisi ya MOI itasiani mkataba wa
ushirikiano na Chuo Kikuu cha Latvia lengo kuu ikiwa ni kubadilishana
uzoefu katika utoaji wa huduma za kibingwa za Usingizi (Anaesthesia)
“Kwa kuanza tutasaini mkataba wa
ushirikiano wa miaka mitatu ambapo watalaamu kutoka hapa watapata fursa
ya kujifunza kwenye Chuo chao lakini pia watakuja hapa kutoa mafunzo ya
muda mfupi kama ambavyo hawa wamekuja” Alisema Dkt Boniface
Dkt Boniface ameongeza kwamba kwa
sasa Taasisi ya MOI imeanzisha huduma ya kulazwa na kufanyiwa upasuaji
siku hiyohiyo yaani (Same day Surgery) hivyo huduma hii itatumika katika
wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji na kuruhusiwa kwani wagonjwa hawapati
maumivu makali baada ya upasuaji na hakuna masharti magumu baada
kufanyiwa upasuaji
Kwa upande wake Profesa Alex
Miscuks kutoka Chuo Kikuu cha Latvia amesema ni heshma kubwa kupata
fursa ya kuja kubadilishana uzoefu hapa Tanzania kwani pamoja na kutoa
mafunzo atapata fursa ya kujifunza mambo mengi.
“Nashukuru sana kwa kunialika,
nimefurahi kukutana na madaktari wazuri na wazoefu hapa MOI, naamimi
mimi pia nitajifunza mambo mengi kwenu, ahsnteni sana” alisema Prof
Miscuks
Kwa upande wake Dkt Iveta Gobovska
ambaye pia ni Mkuu wa kitengo cha wagonja mahututi katika hospitali ya
Chuo Kikuu cha Latvia amesema amefarijika kupata fursa ya kuja
kubadilishana uzoefu na madaktari wa Tanzania na anamini pande zote
mbili zitanufaika na mafunzo haya.
No comments :
Post a Comment