Tuesday, January 29, 2019

MABOMU YARINDIMA NJOMBE


AAA
NJOMBE
Mabomu ya machozi yamelindima katika viunga vya mji wa Njombe kwa lengo la kuwatanya mamia ya wananchi waliokuwa wakiandamana kuelekea kituo kikuu cha polisi cha mkoa wa Njombe wakipinga kitendo cha jeshi hilo kumchukua kinguvu mtu mmoja waliehisia kuwa mtekaji wa watoto , baada ya kumkuta na mtoto mdogo akiwa analia katika mtaa wa mgendela ambapo baada ya wananchi kumuhoji alimuacha mtoto huyo na kutimua mbio.
Wakizungumza na clouds Tv baadhi ya waandamanaji majira ya saa saba mchana akiwemo Pita Remmy na Anitha Mgaya wamesema wamechukizwa na kitendo cha jeshi hilo kuendelea kuwafuga watu hao ambao wamesababisha maisha ya watoto wengi kupotea na kwamba wanamtaka mtuhumiwa huyo waweze wamshughulikie liwe funzo kwa wengine.
Baada ya kurejea kwa hali ya amani katika viunga vya mji wa Njombe,naibu waziri wa mambo ya ndani Mhandisi Hamad Masauni anamtaka kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoa Rashid Ngonyani kueleza sababu ya kupigwa mabomu ambae anasema lengo lilikuwa kumnusuru mtuhumiwa wa wizi wa bodaboda kauli ambayo inapishana na inayotolewa na mkuu wa polisi wilaya ya Njombe Kashilaeli Munuo ambaye amedai mtuhumiwa huyo anahusishwa na utekaji wa watoto.
Mkanganyiko huo unaibua shaka kwa wananchi na kuamua kuweka bayana. Kama ambavyo Alphonce mbulo wanaeleza.
Kufuatia mkanganyiko huo waziri Masauni anawataka wananchi wanaojua chanzo cha kuibuka kwa taaruki hiyo na pindi ukweli utakapo bainika aliyetoa taarifa za uongo mbele ya umma atachukuliwa hatua za kisheria.
Katika maandamano hayo mtu mwanamke mmoja amejeruhiwa na bomu la machozi katika miguu na kukimbizwa katika kituo cha afya cha mjini huku hadi sasa watoto tisa na wengine waliotekwa hawajulikani walipo.

No comments :

Post a Comment