Mkuu
wa wilaya ya Longido Frank Mwaisumbe akiwa na baadhi ya viongozi wa
vijiji na wafanyakazi wa kampuni ya Wingert Windrose Safaris baada ya
kukabidhiwa hundi.
Mwandishi wetu,Arusha.
Meneja
mahusiano ya kampuni hiyo, Clarence Msafiri alimkabidhi Mkuu wa wilaya
ya Longido,Frank Mwaisumbe mfano wa hundi kwa niaba ya vijiji hivyo
kisha kukabidhi hundi halisi yenye thamani ya Sh 3 milioni kwa kila
kijiji.
Vijiji
vilivyonufaika na fedha hizo ni
Mairowa,Magadini,Gelai,Wosiwosi,Ngoswaki na Matale A, Origrai,Matele
B,Lumbwa ,Ilnjakitsapukin ,Kimwati na Alaililai ambapo pia kampuni hiyo
imetoa fedha nyingine kiasi cha dola 5000 zaidi ya sh 11 milioni
kuchangia huduma za jamii kupitia ada ya kitalu chake cha uwindaji.
Akizungumza
baada ya kukabidhiwa hundi hiyo, Mkuu huyo wa Wilaya, Mwaisumbe
aliwataka viongozi wa vijiji kusimamia vizuri matumizi ya fedha hizo
hasa katika kipindi hiki ambacho ujenzi wa madarasa unaendelea kwa kasi
ili kutoa nafasi kwa watoto wa jamii hiyo ya wafugaji kupata fursa ya
elimu.
Mwaisumbe
alisema anaishukuru sana, Kampuni ya Wengert kwa kuwa mdau mkubwa wa
maendeleo katika wilaya hiyo, kutokana na kujitoa kuchangia shughuli
nyingi za maendeleo katika wilaya hiyo.
“Naishukuru
kampuni hii kwa kuonesha uzalendo na kuheshimu makubaliano kusaidia
vijiji na naamini mtaendelea kushirikiana katika kuhakikisha Longido
tunakua na uhifadhi endelevu unaozingatia ustawi wa jamii inazunguka
maliasili zetu,”alisema Mwaisumbe
Meneja
Mahusiano wa kampuni ya Wenget Windrose Safaris Limited,Clarence
Msafiri alisema wataendelea kushirikiana na vijiji vinavyowazunguka
kuchangia huduma za jamii.
Msafiri
alisema licha ya fedha hizo, kampuni hiyo pia itaendelea kutoa ajira
kwa vijana wa jamii inayowazunguka lakini pia tayari wametoa kiasi cha
dola 5000 sawa ni Sh 11.5 milioni ambayo ni malipo kwaajili ya kila
kitalu kila mwaka.
Msafiri
alitaja vijiji vilivyonufaika kuwa ni
Mairowa,Magadini,Gelai,Wosiwosi,Ngoswaki na Matale A,vijiji vingine ni
Origra,Matele B,Lumbwa ,Ilnjakitsapukin ,Kimwati na Alaililai.
Akizungumza
kwa niaba ya vijiji hivyo, Diwani wa Kata ya Mundarara ,Alais Mushao
alisema mchango wa uhifadhi ni muhimu katika kuinua na kuchangia
shughuli za maendeleo na kuitaka kampuni hiyo kufanya kazi zake kwa
kutunza mazingira ili rasilimali hizo zinufaishe vizazi vijavyo.
Kampuni
ya Wingert Windrose Safaris ni kati ya kampuni zinazomilikiwa na
taasisi ya Friedkin Conservation Fund(FCF) ambayo pia inamiliki kampuni
ya Mwiba Holdings iliyowekeza hifadhi ya Makao na Kampuni ya Game
Tracking Safaris(TGTS) ambayo imewekeza maeneo kadhaa nchini.
No comments :
Post a Comment