Katika ghasia hizo, mamia ya masinagogi na biashara zilizokuwa zikimilikiwa na Wayahudi ziliharibiwa na kuchomwa moto, huku mamia kwa maelfu ya Wayahudi wakidhalilishwa hadharani na kufukuzwa nchi. ambapo inadhaniwa kuwa takribani Wayahudi 100 waliuawa katika machafuko hayo.
Aidha, kuzinduliwa kwa kampeni hiyo ya uhalifu uliofanywa na utawala wa Kinazi dhidi ya Wayahudi walioishi Ujerumani, baadaye kulitambulika kama usiku wa Kioo Kilichovunjika, kwa kuwa mitaa yote ilifunikwa na vifusi vya vioo vya madirisha ya mali zilizomilikiwa na Wayahudi, ambayo yaliharibiwa vibaya.
No comments :
Post a Comment