Thursday, November 15, 2018

STARTMIMES YAJA NA LIPA TUKUBUSTI MSIMU WA KRISMASI


Capture
Meneja masoko wa Startimes Davis Malisa akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa promosheni mpya kabambe kabisa awa wateja wao pendwa kwenye msimu huu wa Krismasi uliofanyiaka jijini Dar es Salaam.
02
 Meneja Maudhui wa Startimes Zamaradi Nzowa akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali wa tasnia ya Filamu pamoja na muziki wa kuhusu maudhui zitakazopatikana kwenye vifurushi vya Startimes wakati wa uzinduzi wa promosheni mpya kabambe kabisa awa wateja wao pendwa kwenye msimu huu wa Krismasi uliofanyiaka jijini Dar es Salaam.
2
Mkurugenzi wa Benchmark Production, Rita Paulsen akizungumza kuhusu Startimes wanavyoshirikiana kwenye kuibua vipaji vya wasanii wachanga wakati wa uzinduzi wa promosheni mpya kabambe kabisa awa wateja wao pendwa kwenye msimu huu wa Krismasi uliofanyiaka jijini Dar es Salaam.
3
Picha ya Pamoja
……………………
“…Kwa wateja wetu pendwa kabisa, na wale ambao bado hawajajiunga na familia ya StarTimes inayokua kila siku, msimu huu wa siku kuu tunawaletea ‘LIPA TUKUBUSTI’ambayo inakupatia faida nne. Katika kila utakachonunua kutoka kwetu basi sisi
tutakuBUSTI ama tutakuongezea.”
Dar es Salaam Novemba 14, 2018.
Kampuni ya Star Media (T) Ltd kupitia chapa yake ya StarTimes wametangaza ujio wa Promosheni ya LIPA TUKUBUSTI katika msimu huu wa Siku Kuu. Promosheni hiyo imezinduliwa Alhamisi ya wiki hii kwatika Ukumbi wa Terrace, Slipway Masaki jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na waigizaji maarufu wa Bongo Movie pamoja na wasanii wa Muziki wa kizazi Kipya.
Katika Promosheni ya LIPA TUKUBUSTI wateja wa StarTimes watakuwa wakipatiwa vifurushi vikubwa zaidi kila watakapolipia na kujiunga na vifurushi vyao vya kawaida kwa malipo ya mwezi Mzima. Hali kadhalika kwa wateja wapya watapatiwa Antena BUREE kila watakaponunua king’amuzi cha Antenna kwenye maduka na mawakala wa StarTimes.
“Vifurushi vyetu, kwa wateja wa Antenna Ukilipia kifurushi cha NYOTA kwa Tsh 8,000/= utapata kifurushi cha MAMBO kwa mwezi mzima, Ukilipia kifurushi cha MAMBO kwa Tsh 14,000/= tutakuBUSTI hadi kifurushi cha UHURU kwa mwezi mzima, na ukilipia UHURU utapatiwa wiki moja BUREEE!!”. Ndg David Malisa Meneja Masoko wa StarTimes
“Ving’amuzi vyetu, pata Antena ya BURE ukinunua king’amuzi cha Antenna kwa Tsh 99,000/= tu, au furahia kifurushi cha SUPER mwezi mzima BUREEE utakaponunua king’amuzi cha Dish wa Tsh 106,000/= tu. Huu ndio wakati sahihi zaidi kwa wewe ambaye bado hujajiunga nasi kununua king’amuzi chako, kwani unapataza ZAIDI kila unapolipia”. Aliongeza Bw. Malisa.
Sio hivyo tu bali kupitia promosheni ya LIPA TUKUBUSTI wateja watanufaika kwa Kupata DISH la BUREEE kila watakaponunua luninga za Kidigitali za StarTimes za ukubwa wowote ule kuanzia Inchi 24, 32, 43 hadi ile Luninga Smati ya Inchi 55.
Kwa upande wa maudhui, Msimu huu wa Siku Kuu StarTimes wamejipanga vilivyo kwani wanaleta Filamu Mpya kabisa za Bongo Movie zilizosheheni mastaa wakali, Huku shindano la Bongo Star Search likiendelea, na kufikia hatua ya mchujo ndani ya Studio, Shindano hilo linaendelea kuonekana Kila siku saa tatu Usiku kupitia chaneli ya StarTimes Swahili Pekee.
“Tuna furaha kubwa kuwaletea filamu za Bongo Movie Mpya kabisa kwa mwezi mzima wa Disemba, filamu ambazo zina mastaa tunawaowapenda na kuwafatilia kila siku. Ni wakati wa kutengeneza kumbukukumbu nzuri na wale tuwapendao na StarTimes inalifanikisha hilo. Sio hayo tu bali tunaleta Msimu mpya wa Coppa Italia kwa mara ya kwanza kupitia StarTimes pekee, utamshuhudia Cristiano Ronaldo na Juventus kuanzia Disemba 5 kupitia chaneli zetu za Michezo”. Zamaradi Nzowa Meneja Maudhui, StarTimes.
Pia ligi ya Bundesliga inayoonyeshwa na StarTimes pekee, inaendelea sambamba na ligi ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1, huku zikichagizwa na Ligi ya EUROPA. Bila kusahau chaneli na vipindi vya watoto kama Jim Jam, POP na chaneli mpya ya ST Kids vitahakikisha watoto wako wanakuwa na siku kuu ya kipekee.
Kuhusu StarTimes
StarTimes ni kampuni ya Matangazo ya kidigitali inayoongoza Africa, ikihudumia zaidi ya wateja milioni 10 katika bara zima. StarTimes inamiliki jukwaa la maudhui lenye chaneli zaidi ya 480 zikiwemo chaneli za Habari, filamu, tamthiliya, michezo, burudani, vipindi vya watoto, mitindo, dini na vingine vingi. Matazamio ya Kampuni ni “Kuhakikisha kila familia ya kiafrika inapata, inamudu, inatazama na kushiriki kwenye Uzuri wa Televisheni ya kidigitali”

No comments :

Post a Comment