Thursday, September 20, 2018

ZIARA YA WAZIRI MKUU WILAYANI KONDOA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Mkuu wa Mkoa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge, alipowasili katika kituo cha afya cha Mauno Wilayani Kondoa, akiwa kwenye ziara yake ya kikazi Mkoani Dodoma, Septemba 20, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiangalia chumba cha kuhifadhia maiti, wakati alipokagua ujenzi wa kituo cha afya cha kata ya Mauno Wilayani Kondoa Mkoani Dodoma, Septemba 20, 2018, kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma Godwin Mkanwa, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Dk. Ikaji Rashid. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 Wananchi wa Kata ya Mauno wilayani Kondoa, wakimsikiliza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipowasili katika kata hiyo akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Dodoma, Septemba 20, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza wananchi wa Kata ya Mauno wilayani Kondoa, akiwa kwenye ziara yake ya kikazi Mkoani Dodoma, Septemba 20, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, akizungumza na wananchi wa Kata ya Mauno Kondoa Mkoani Dodoma, Septemba 20, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments :

Post a Comment