Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista
Mhagama (Mb) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua
zilizochukuliwa na Serikali katika katika kujenga uchumi wa viwanda
ikiwemo kufuta baadhi ya tozo zilizokuwa zikitozwa na Wakala wa Usalama
na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA) ikiwemo ada ya Leseni ya kukidhi matakwa
ya Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi hii leo Jijini Dodoma
Septemba 20, 2018.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa
Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA) Bi. Hadija Mwenda akizungumzia
umuhimu wa kulinda afya na Usalama kwa wafanyakazi katika maeneo ya
kazi wakati wa mkutano wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,
Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (Mb) na
waandishi wa habari leo Jijini Dodoma.
Mkuu wa Kitengo Cha Sheria kutoka
Wakala wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA) Bi. Joyce Mwambungu
akifafanua kwa waandishi wa habari juu ya baadhi ya Tozo za kikanuni
ambazo zimefutwa kwa mujibu wa Sheria. (Kushoto) ni Kaimu Mtendaji Mkuu
wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA) Bi. Hadija Mwenda na
Mkurugenzi wa Usalama na Afya (OSHA) Bw. Alex Ngata.
Baadhi ya waandishi wa habari
wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge,
Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo
pichani) alipokutana nao hii leo kuzungumzia hatua zilizochukuliwa na
Serikali katika katika kujenga uchumi wa viwanda ikiwemo kufuta baadhi
ya tozo zilizokuwa zikitozwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi
(OSHA) leo Jijini Dodoma.
Sehemu ya waandishi wa habari
wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge,
Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo
pichani) alipokutana nao hii leo kuzungumzia hatua zilizochukuliwa na
Serikali katika katika kujenga uchumi wa viwanda ikiwemo kufuta baadhi
ya tozo zilizokuwa zikitozwa na Wakala wa
Usalama na Afya Mahala Pa Kazi
(OSHA).
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu
……………….
Na.Alex Sonna wa Fullshangweblog,Dodoma
Serikali imeamua kufuata baadhi ya
Ada na Tozo mbalimbali zisizoondoa wajibu kutoka kwa muajiri kwa ajili
ya kulinda Afya za Wafanyakazi ili kuweza kuvutia na kuchochea Ujenzi wa
Uchumi wa Viwanda kwa lengo la kuimarisha Maendeleo nchini .
Akizungumza na Waandishi wa habari
Jijini Dodoma Wazari wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu,Sera,Bunge,Kazi,Vijana na Wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama amesema
kuwa mabadiliko hayo yalifanywa kutoka katika Mamlaka ya Usalama na
Afya inayohusiana na OSHA kwa Lengo la kuchangia na kutekeleza azma ya
Serikali ya awamu ya tano kuyaweka mazingira salama kwa wawekezaji.
”Tumeamua kufuta baadhi ya Ada
zikiwemo Ada ya kuchukua fomu ya Usajili ambayo gharama yake ilikuwa
shilingi 2000 pamoja na Ada ya usajili wa maeneo ya kazi kwa kuzingatia
ukubwa wa Eneo ambayo nayo ilikuwa gharama zake ni shilingi
50,000,80o,000 hadi 1,000,000 kwa sasa maeneo hayo ni bure” amesema
Mhe.Mhagama
Pamoja na hayo Waziri
Mhagama,amesema kuwa wameamua pia kufuta Ada ya Leseni ya kukidhi
matakwa ya Sheria ya Usalama na Afya Mahala Pa Kazi ambayo pia ilikuwa
ikitozwa kwa Gharama ya shilingi 200,000 kwa mwaka kwa ajili ya
kuimarisha na kuboresha mazingira ya kufanyia biashara kwa sasa leseni
hiyo nayo ni bure.
Kwa Upande Wake Joyce Mwambungu
Mkuu wa Kitengo cha Sheria Katika Afya Salama,amesema kuwa OSHA kwa sasa
imewekeza nguvu za kutoa Elimu kwa wadau kuhusu tamko la Kisheria la
kulinda Afya za Wafanyakazi nchini Mahala Pa Kazi katika Sekta
mbalimbali ili kuweza kusimamia mifumo ya Utendaji wa watumishi ili
kuondoa Mianya ya Rushwa ili kufanikisha uwazi na uwajibikaji
”Sisi jukumu kubwa zaidi ni kutoa
mafuzo na Elimu kwa jamiii ili iweze kujua na kujifunza kwa kupitia
Elimu kwa wadau wote nchini ili Takwa hili la kisheria liweze kufanikiwa
kwa Kulinda Afya za Wafanyakazi nchi Mahala Pa Kazi na OSHA ipo tayari
kuhakikisha uchumi wa viwanda unakuwa na kuleta tija kwa Taifa
Letu”amesema Mwambungi
No comments :
Post a Comment