TAARIFA KWA UMMA
MAADHIMISHO YA SIKU YA MOYO DUNIANI
TAREHE 29/09/2018
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kuwajulisha wananchi kwamba itafanya upimaji na utoaji wa elimu ya afya ya moyo bila malipo katika Hospitali
ya Vijibweni iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam. Upimaji huu
utafanyika kwa watoto na watu wazima kuanzia saa 2 (mbili) asubuhi.
Wananchi wote mnakaribishwa.
Kauli mbiu: “Kwa moyo wangu, kwa moyo wako, sote pamoja kwa mioyo yetu , tunatimiza ahadi”.
Limetolewa na:
Kitengo cha Uhusiano
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
No comments :
Post a Comment