Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
na Balozi wa Japan nchini Mhe. Masaharu Yoshida pamoja na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi)
Mhe. Elias Kwandikwa akimpongeza Mtendaji Mkuu
wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Mhandisi Patrick
Mfugale baada ya kuzindua rasmi Daraja la Juu la Mfugale
(Mfugale Flyover) katika makutano ya barabara za Nyerere na Mandela
maeneo ya
TAZARA jijini Dar es salaam leo Septemba 27, 2018. Rais alimwagia sifa
Mhandisi Mfugale na kumwita kuwa ni Mtanzania muaminifu kwa taifa lake
ambapo amechangia pakubwa katika usimamizi wa ujenzi wa miundombinu
mikubwa na mkidogo hapa nchini kwa umahiori mkubwa na kutanguliza mbele
maslahi ya taifa na siyo binafsi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akihutubia wakati akizindua rasmi wa Daraja la Juu la Mfugale (Mfugale
Flyover) katika makutano ya barabara za Nyerere na Mandela maeneo ya TAZARA
jijini Dar es salaam leo Septemba 27, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
na Balozi wa Japan nchini Mhe. Masaharu Yoshida akipena mikono na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi)
Mhe. Elias Kwandikwa baada ya kuzindua rasmi Daraja la Juu
la Mfugale (Mfugale Flyover) katika makutano ya barabara za Nyerere na Mandela
maeneo ya TAZARA jijini Dar es salaam leo Septemba 27, 2018.
Mke wa Rais Dkt. Magufuli, Mama Janeth Magufuli, akiongozana na Shekhe
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na mwakilishi wa BAKWATA Sheikh Alhad Mussa Salum
wakielekea kushuhudia uzinduzi rasmi wa Daraja la Juu la Mfugale (Mfugale
Flyover) katika makutano ya barabara za Nyerere na Mandela maeneo ya TAZARA
jijini Dar es salaam leo Septemba 27, 2018.
Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ukipita katika Daraja la Juu la Mfugale (Mfugale Flyover) katika makutano ya barabara za Nyerere na Mandela maeneo ya TAZARA jijini Dar es salaam baada ya uzinduzi rasmi leo Septemba 27, 2018. (PICHA NA IKULU)







No comments :
Post a Comment