Friday, September 28, 2018

NBC MDHAMINI MKUU MAONYESHO YA MADINI GEITA


????????????????????????????????????
Ofisa wa Huduma kwa wateja wa Benki ya NBC, Pili Salum akizungumza na watoto wa Shule ya Msingi Nyanza wakati wa maonyesho ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayoendelea katika Viwanja vya CCM Kalangalala mkoani Geita.
????????????????????????????????????
Ofisa Mahusiano ya Wateja wa Benki ya NBC, Esther Kahabi  akizungumza na wakazi wa Geita pamoja na wafanyakazi wa migodini wakati wa maonyesho ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayoendelea katika Viwanja vya CCM Kalangalala mjini Geita.
????????????????????????????????????
Meneja wa Kanda ya Ziwa wa Benki ya NBC, Japhet Mazumira (kushoto) akizungumza na kikundi cha wajasiriamali wadogo wadogo mafundi viatu walemavu baada ya kutembelea katika banda lao wakati wa maonyesho ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayofanyika  katika Viwanja vya CCM Kalangalala mkoani Geita.
????????????????????????????????????
Ofisa Mauzo wa Benki ya NBC, Joseph Boaz (kulia) akizungumza na wakazi wa Geita pamoja na wafanyakazi wa migodini wakati wa maonyesho ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayofanyika katika Viwanja vya CCM Kalangalala mjini Geita.
????????????????????????????????????
Meneja Mahusiano wa Benki ya NBC, William Kallaghe (wa pili kushoto), akitoa maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo kwa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kushoto) wakati naibu waziri huyo alipokwenda kuzindua rasmi maonyesho ya kwanza ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini Mkoani Geita juzi. NBC ilikuwa ni mdhamini mkuu wa maonyesho hayo. Wengine kutoka kulia ni Meneja wa NBC Geita, Martin Nkanda,   Meneja wa Kanda ya Ziwa, Japhet Mazumira na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati, Evance Luhimbo
????????????????????????????????????
Meneja Uhusiano wa Benki ya NBC, William Kallaghe (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi  Gabriel Robert (wapili kulia) baada ya kutembelea katika banda la Benki hiyo wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Teknolojia na uwekezaji kwenye sekta ya madini yaliyofanyika katika viwanja vya CCM Kalangalala jijini Geita juzi. Wengine ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya maonyesho, Chacha Wambura na Meneja wa NBC Geita, Martin Nkanda.
????????????????????????????????????
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi  Gabriel Robert (kulia)  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka (wapili kulia) na Meneja Mahusiano wa Benki ya NBC, William Kallaghe wakitembelea moja ya mabanda ya wajasiriamali  katika maonyesho ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini mjini Geita jana. NBC ilikuwa ni mdhamini mkuu wa maonyesho hayo.

No comments :

Post a Comment