Friday, September 28, 2018

NAIBU WAZIRI NDUGULILE ATEMBELEA TAASISI YA USTAWI WA JAMII


IMG_2294
Mh. Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile  akipokelewa na Kaimu Mkuu wa Taasisi Ya Ustawi wa Jamii  Dkt Zena Mabeyo alipofika kutembelea Taasisi hiyo.
IMG_2342
Mh. Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dkt. faustine Ndugulile Akiongea na watumishi wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii.
IMG_2314
Mh Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto akisikiliza ripoti ya utendaji kazi wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Taasisi Dkt. Zena Mabeyo.
IMG_2323
Wajumbe wa menejimenti ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii wakimsikiliza Mh. Naibu waziri Dkt. Faustine Ndugulile wakati alipokutana nao Jana.
Mh. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) Naibu waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto leo tarehe 27/09/2018 amefanya ziara katika Taasisi ya Ustawi wa Jamii ikiwa ni
miongoni mwa ziara za kutembelea taasisi zilizo chini ya wizara yake katika kuboresha utendaji kazi.
Dkt Ndugulile amefanya mkutano na menejimenti, wafanyakazi pamoja na viongozi wa  serikali ya wanafunzi wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii ambapo pamoja na mambo mengine Mh Naibu Waziri alisomewa taarifa ya maendeleo ya taasisi na mipango ya baadae.
“Nimeskia taarifa nzuri ya maendeleo na mafanikio pamoja na changamoto za Taasisi, nawaagiza viongozi kutatua changamoto ambazo ziko ndani ya uwezo wenu na sisi kama serikali tutazifanyia kazi zile zinazotuhusu. Lengo letu ni kuhakikisha kuwa huduma zinaendelea kutolewa kwa ubora na maslahi ya watumishi yanaboreshwa”. Alisema Dkt. Ndugulile.
Aidha Mh. Naibu waziri Ndugulile ametoa maagizo kwa menejimenti ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii kufanyia kazi kwa muda mwezi mmoja tu,baadhi ya mambo ambayo ameona yanahitaji ufumbuzi wa mapema ili kuboresha mazingira ya utoaji huduma katika Taasisi ya Ustawi wa Jamii.
Katika kuhitimisha mkutano wake na uongozi, wafanyakazi pamoja na serikali ya wanafunzi wa Taasisi, Mh. Naibu Waziri Dkt. Ndugulile amepongeza kazi nzuri inayofanywa na watumishi na ameahidi wizara kuendelea kushirikiana na Taasisi ya Ustawi wa jamii katika kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji ya wananchi.

Imetolewa na:
Benedict Nkwao
Afisa Uhusiano
Taasisi ya Ustawi wa  Jamii
Dar es Salaam

No comments :

Post a Comment