Katibu
Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi
Mhandisi, Balozi John Kijazi akizungumza katika Kikao Kazi cha siku tatu
cha Makatibu Wakuu, Makatibu Tawala wa Mikoa na Manaibu Katiku Wakuu wa
wizara kilichoanza jana tarehe 19 Septemba 2018 jijini Dodoma.(Picha
na: Frank Shija - MAELEZO)
Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhandisi, Balozi John
Kijazi(kushoto) akiteta jambo na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu
Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzabar, Dkt. Adulhamid Yahya
Mzee wakati wa Kikao Kazi cha siku tatu cha Makatibu Wakuu, Makatibu
Tawala wa Mikoa na Manaibu Katiku Wakuu wa wizara kilichoanza jana
tarehe 19 Septemba 2018 jijini Dodoma.
Baadhi ya washiriki wa Kikao Kazi
cha siku tatu cha Makatibu Wakuu, Makatibu Tawala wa Mikoa na Manaibu
Katiku Wakuu wa wizara wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu Kiongozi
Balozi, Mhandisi John Kijazi (hayupo pichani) wakati wa kikao hicho
kilichoanza jana tarehe 19 Septemba 2018 jijini Dodoma. (Picha na: Frank
Shija –MAELEZO).
Na:Frank Mvungi- MAELEZO
Miundo mipya ya Wizara na Taasisi
za Serikali kuongeza ufanisi na kupunguza gharama za uendeshaji wa
Serikali hali inayoongeza kasi ya kutoa huduma Bora kwa wananchi hasa
wale wanyonge.
Akizungumza wakati wa Kikao Kazi
cha Makatibu Wakuu, Makatibi Tawala wa Mikoa na
Manaibu Katibu Wakuu wa
Wizara kinachofanyika Jijini Dodoma, Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi
Balozi John Kijazi amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imeazimia
kujenga uchumi wa Viwanda utakaowanufaisha wananchi wote.
“ Mikutano hii itakuwa ikifanyika
kila mwaka baada ya kutofanyika mwaka 2016 na mwaka 2017 kutokana na
zoezi lililokuwa linaendelea la kupanga upya safu ya watendaji Wakuu
ndani ya Serikali na Taasisi zake katika Serikali mpya ya Awamu ya Tano,
pamoja na kuboresha mifumo ya uendeshaji wa Serikali” ; Alisisitiza
Akifafanua Balozi Kijazi amesema
kuwa kwakuzingatia dhamira ya Serikali ni dhahiri kuwa lengo la kufikia
uchumi wa kati litafikiwa katika muda uliopangwa.
Aliongeza kuwa Watendaji wote
Serikalini wanapaswa kusoma na kuelewa mazingira ya sasa na kutekeleza
majukumu yao kulingana na mipango, maelekezo na mahitaji ya wakati huu
wa Serikali ya Awamu ya Tano, na azma ya Kiongozi wetu Mkuu, Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Pia Balozi Kijazi aliwaasa
washiriki wa Kikao Kazi hicho kuepuka tabia ya kufanya kazi kwa mazoea
kama ilivyozoeleka huko nyuma kwa kuzingatia sheria , Kanuni na Taratibu
za Serikali ya Awamu ya Tano kwa maslahi ya wananchi.
Katika Kikao Kazi hicho mada
mbalimbali zinawasilishwa ikiwemo ; Uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na
Miongozo, Matumizi ya TEHAMA Serikalini, Utawala Bora na Mapambano Dhidi
ya Rushwa, Ulinzi na Usalama, Mkakati, Mwongozo na Mwelekeo kuhusu
agenda ya Tanzania ya Viwanda na mifumo ya Udhibiti wa ndani Serikalini
na jumuiya za Kiraia.
Kikao Kazi cha Makatibu Wakuu na
Makatibu Tawala wa Mikoa kinafanyika Jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya
mikakati ya Serikali kuimarisha utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma
bora kwa wananchi hasa wanyonge ili kutimiza azma ya Serikali ya Awamu
ya Tano inayoongozwa na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kujenga Tanzania
mpya.Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na
Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Abdulhamid
Yahya Mzee.
No comments :
Post a Comment