Mkurugenzi wa Bodi akiwa pia
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Mohammed Omar Bin Haider Holding Group (MOBH) ,
Bwana Omar Mohammad Bin Haider Kulia akibadilishana mawazo na Makamu wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kabla ya utiaji saini Mkataba wa
Makubalizno ya kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika masuala ya kuimarisha Uwekezaji.
Waziri wa Fedha wa Zanzibar Dr.
Khalid Salum Mohamed kulia na Mkurugenzi wa Bodi akiwa na Meneja Mkuu
wa Kampuni ya Mohammed Omar Bin Haider Holding Group -MOBH, Bwana Omar
Mohammad Bin Haider, wakiwa katika Hoteli ya Kimataifa ya Grand Exelsior
iliyopo katika mji wa Al – Brsha Dubai wakitia saini mkataba wa
makubaliano ya kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika masuala ya kuimarisha uwekezaji.
Wa kwanza kutoka Kulia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akishuhudia tukio hilo la Kihistoria kwa Zanzibar katika harakati za kunyanyua uchumi wake.
Wa kwanza kutoka Kulia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akishuhudia tukio hilo la Kihistoria kwa Zanzibar katika harakati za kunyanyua uchumi wake.
Dr. Khalid Kulia na Bwana Omar
Mohammad Bin Haider wakibadilishana hati ya Mkataba mara baada ya
kuusaini wa kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
katika masuala ya kuimarisha Uwekezaji.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi kulia akimpongeza Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo
Bwana Omar Mohammad Bin Haider baada ya kukamilisha zoezi la kutia
saini, Waziri wa Fedha wa Zanzibar Dr. Khalid kati kati akishuhudia.
Waziri wa Fedha wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Dr., Khalid Salum Mohamed akitoa Hotuba katika
chakula Maalum cha Mchana kilichoandaliwa na Kampuni Bwana Omar Mohammad
Bin Haider mara baada ya kumalizika kwa hafla ya utiaji saini.
Kampuni ya MOBH Holding Group
Bwana Omar Mohammad Bin Haider mwenye Kilemba katikati kulia yake
Balozi Seif na kushoto yake Dr. Khalid wakiwa katika picha ya pamoja na
viongozi na watendaji wa Kampuni hiyo na Wanabalozi wa Tanzania nchini
Dubai mara
baada ya kukamilika kwa zoezi la utiaji saini.
Safari ya Zanzibar kuelekea katika
mtazamo wa matarajio ya kuwa Dubai ya Afrika Mashariki inaanza kuchipua
kufuatia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutiliana saini Mkataba na
Kampuni ya Kimataifa ya Mohammed Omar Bin Haider Holding Group (MOBH )
ya Nchini Dubai.
Saini ya Mkataba huo ilitiwa baina
ya Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar Dr. Khalid Salum Mohamed
ambaye alitia saini hiyo kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
wakati Bwana Omar Mohammad Bin Haider wa Kampuni ya Mohammed Omar Bin
Haider Holding Group ilitiwa na Mkurugenzi wa Bodi akiwa pia Meneja Mkuu
wa Kampuni hiyo Bwana Omar Mohammad Bin Haide, hafla iliyofanyika
katika Hoteli ya Kimataifa ya Grand Exelsior Mjini Al Barsha Nchini
Dubai, imelenga kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika masuala ya kuimarisha uwekezaji na maendeleo ya Zanzibar
Kiuchumi.
Hafla hiyo ilishuhudiwa pia na Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyetokea Nchini China kuhudhuria
Maonyesho ya 15 ya Kimataifa ya China- Asean Expo 2018 yaliyofanyika
katika Mji waNanning katika Jimbo la Guangxi.
Akizungumza mara baada ya utiaji
saini mkataba huo Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dr. Khalid Salum
Mohamed alisema Zanzibar imeahidi na kuwa tayari kuiona Kampuni hiyo
yenye Makao Makuu yake Nchini Dubai inazitumia furza za Uwekezaji
zilizopo Visiwani Zanzibar ambapo ndipo palipokuwa kitovu cha harakati
za Kibiashara kilichokuwa kikiunganisha Bara la Asia na Ukanda wa Kusini
na Mashariki mwa Bara la Afrika lenye wakaazi zaidi ya Milioni
360,000,000, kwa hivi sasa imepania kuirejeshea hadhi yake kwa kutanua
maeneo mengine ya Uwekezaji.
Aisema Miundombinu iliyoimarishwa
katika Sekta za Mawasiliano ya Anga, Uvuvi wa Bahari Kuu, Utalii na
Biashara ikiambatana na Sera inayotekelezeka imezingatia kuwajengea
mazingira bora awekezaji wa Ndani na Nje kuwekeza Miradi yao katika
mfumo wa makubaliano ukiwemo ule wa Ubia. “ Tunakaribisha wawekezaji wa
kigeni zaidi katika kusaidia kuimarisha uchumi wa Zanzibar hasa katika
sekta ya Utalii inayounganishwa hivi sasa na safari za moja kwa moja za
anga kutoka maeneo mbalimbali ya Dunia”. Alisema Dr. Khalid Salum.
Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar aliueleza uongozi huo wa
Kampuni ya MOHB Holding Group kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
katika juhudi za kuimarisha Uchumi wake imeanzisha maeneo mengine ya
uwekezaji ili kutanua wigo wa uchumi wake ambayo ni mradi mpya wa
utafiti wa Mafuta na Gesi Asilia unaoendelea pamoja na matayarisho ya
ujenzi wa Bandari ya Mizigo ya Mpiga Duri maeneo ambayo Kampuni hiyo
inaweza kufikiria namna ya kusaidia kwake.
Alisema Dira ya Maendeleo ya 2025 na Mpango wa Maendeleo 2020
imelenga kuinyanyua Zanzibar kiuchumi ili wananchi wake wafikie hatua ya
ustawi uliotukuka, mipango ambayo inayohusishwa pia na Taasisi, Mataifa
na Mashirika ya Maendeleo ya ndani na nje ya Nchi.
Dr. Khalid alifahamisha kwamba
Kampuni ya Mohammed Omar Bin Haider Holding Group kutokana na uzoefu
wake wa muda mrefu uliyonayo na mtandao mzuri wa uwekezaji bado wana
fursa ya kuangalia maeneo zaidi wanayoweza kufikiria kuwekeza Zanzibar.
Aidha Uongozi wa Kampuni hiyo
umeridhika na ukarimu mkubwa walionao Watu wa Visiwa vya Zanzibar wakati
wa ziara ya ujumbe huo uliyoifanya Zanzibar mwishoni mwa Mwezi Agosti
2018 ambao umeshawishika kutaka kuwekeza miradi yao ya kiuchumi Visiwani
Zanzibar.
Katika kuunga mkono jitihada za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye uimarishaji wa Uchumi wake
Taasisi hiyo ya Uwekezaji imeonyesha nia ya kuwasilisha maombi yake ya
kutaka kuwekeza miradi katika sekta mbalimbali zikiwemo za Mawasiliano,
uvuvi wa Bahari Kuu, Kilimo pamoja na Viwanda.
Kampuni ya MOHB Holding Group
yenye Makampuni tofauti zaidi ya Sita katika Mataifa mbali mbali ya
Mashariki ya Kati inajishughulisha zaidi na Miradi mbali mbali ya
Ujenzi wa Miji ya Kisasa, Huduma za Afya, Elimu, Miundombinu, Biashara
pamoja na Sekta ya Utalii.
Muungano wa Nchi za Falme za
Kiarabu (UAE) imewekeza Nchini Tanzania Miradi mbali mbali ya Kiuchumi
inayokadiriwa kuwa na gharama ya Dola za Kimarekani Milioni 991 kuanzia
Mwaka 2003.
Habari na Picha kwa hisani ya:-
Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
Ofisi ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki-Zanzibar.
19/09/2018.
No comments :
Post a Comment