Monday, September 10, 2018

IBADA YA KUWEKA JIWE LA MSINGI WA UJENZI NA UZINDUZI WA KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA (KKKT) DAYOSISI YA MASHARIKI NA PWANI JIMBO LA KUSINI MTAA WA MWAPEMBA


  Waumini wa Kanisa la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani Jimbo la Kusini Mtaa wa Mwapemba wakiwa katika ibada ya kuwekwa jiwe la msingi wa ujenzi wa kanisa na uzinduzi wa mtaa iliyofanyika jana katika kanisa hilo lililopo Temeke jijini Dar es Salaam.


NA ANNA NKINDA

WAUMINI wa Kanisa la  Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) wametakiwa kumtegemea  Mungu katika maisha yao na kuacha tabia ya kuhama hama makanisa kwa kudhani kuwa  huko wanakokwenda ni kuzuri zaidi ya mahali walipotoka.

Rai hiyo imetolewa jana na Mkuu wa  Jimbo la Kusini kutoka Dayosisi ya Mashariki na Pwani Mchungaji Andrew King’homella  wakati wa ibada ya kuwekwa kwa jiwe la msingi pamoja na uzinduzi wa Mtaa wa Mwapemba uliopo wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Mchungaji King’homella  alisema  Mungu yuko kila mahali jambo la muhimu ni kwa mkristo kusoma biblia na  kuifahamu,  kumwomba  Mungu katika roho na kweli na  kumsikiliza Mungu kwa kufanya hivyo Mungu atasikia na kujibu maombi yake.

“Wakristo wengi wamekuwa ni watu wa kuvunjika moyo hasa wanapokutana na matatizo mbalimbali wanafikiri kwa kuhama makanisa shida zao zitakwenda kumalizika, wanasahau kuwa  Mungu yupo hata pale wanapoabudu”.

“Ukimtegemea Mungu kwa neema yake hata kama unateseka kwa magonjwa na matatizo mengi wakati wako ukifikaa atakuponya haijalishi uko mahali gani”, alisisitiza Mchungaji King’homella .

Akisoma risala ya ujenzi wa kanisa hiko Mwenyekiti wa Kamati ya majengo David Kisai alisema mtaa huo ulianza mwaka mwezi wa kumi mwaka 2013 kwa kuwa na waumini  13 kati ya  hao watu wazima tisa na watoto wa nne ambapo ibada zilikuwa zinafanyika katika moja ya nyumba ya muumini. Hivi  sasa kuna jumla ya waumini 187 kati ya hao watu wazima 127 na watoto 60.

“Jengo hili likikamilika litakuwa na uwezo wa kuchukuwa waumini 300 katika ibada moja na litakuwa na vyumba vitano vya ofisi ambavyo ni ofisi za mchungaji, Mwinjilisti, Parish worker na ofisi nyingine mbili zitatumika kwa matumizi mbalimbali ya kanisa” alisema Kisai.
Ibada hiyo ilienda sambamba na harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo ambapo jumla ya shilingi milioni 25 zilipatikana huku malengo yakiwa ni kuchangisha milioni 50 fedha ambazo zitatumika kukamilisha ujenzi wa boma pamoja na kuezeka.
  Mkuu wa Jimbo la Kusini  wa Kanisa la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani Mchungaji Andrew King’homella  akiweka  jiwe na msingi  la ujenzi wa Kanisa na uzinduzi wa  Mtaa wa Mwapemba katika ibada iliyofanyika jana kwenye kanisa hilo lililopo Temeke jijini Dar es Salaam.

  Mkuu wa Jimbo la Kusini  wa Kanisa la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani Mchungaji Andrew King’homella  akifanya maombi  kabla ya kuweka  jiwe na msingi  la ujenzi wa Kanisa na uzinduzi wa  Mtaa wa Mwapemba katika ibada iliyofanyika jana kwenye kanisa hilo lililopo Temeke jijini Dar es Salaam.

Waumini wa Kanisa la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani Jimbo la Kusini Mtaa wa Mwapemba wakilizunguka kanisa lao huku wakiimba kabla ya kuanza kwa ibada ya kuwekwa jiwe la msingi wa ujenzi wa kanisa na uzinduzi wa mtaa iliyofanyika jana katika kanisa hilo lililopo Temeke jijini Dar es Salaam.

  Kibao cha jiwe la msingi la ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani Jimbo la Kusini Mtaa wa Mwapemba kama kinavyoonekana katika picha.


Waumini wa Kanisa la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani Jimbo la Kusini Mtaa wa Mwapemba wakilizunguka kanisa lao huku wakiimba kabla ya kuanza kwa ibada ya kuwekwa jiwe la msingi wa ujenzi wa kanisa na uzinduzi wa mtaa iliyofanyika jana katika kanisa hilo lililopo Temeke jijini Dar es Salaam.(PICHA NA ANNA NKINDA)

No comments :

Post a Comment