WAZIRI
wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ambaye
pia ni Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga{CCM) akiwa kwenye picha ya
pamoja na wanafunzi wa shule ya Sekondari Toledo mara baada ya
kuwakabidhi madawati 40
|
NA MWANDISHI WEYTU
WAZAZI
kote nchini wametakiwa kuacha kulalamikia wadau wa elimu na badala yake
wameshauriwa kushirikiana na walimu kukagua madaftari ya watoto wao kwa
lengo la kuongeza ufaulu ili kupunguza mimba za utotoni zinazosababisha
ndoto zao kushindwa kufikiwa.
Hayo
yalisemwa na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto
Ummy Mwalimu wakati halfa ya kukabidhiano ya madawati na viti vyake 40
aliyoyatoa kwenye shule ya Sekondari Toledo ya Jijini Tanga.
Ummy
ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu kupitia chama cha Mapinduzi {CCM) mkoa
wa Tanga alisema kimsingi wazazi wanapaswa kutambua kufanya hivyo
kutawasaidia kuwawezesha vijana wao kuongeza ufaulu na hivyo kufanikiwa
kuepukana na vishawishi ambavyo wanakabiliana navyo wakati wakiwa
shuleni.
“Ndugu
zangu wazazi na walezi lazima tutambue jukumu letu la kufuatilia
maendeleo ya watoto wetu kwani hii ndio njia pekee inayoweza kuwasaidia
kwa kushirikiana na walimu wao kwa lengo la kuwezesha kufikia ndoto
zao”Alisema. Naye
ka upande wake Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa aliwataka
wanafunzi kutumia fursa hiyo kuongeza jitihada kwenye kusoma ili azma ya
serikali ya kuongeza ufaulu kwa shule zake iweze kufikiwa.
“Ndugu
zangu wanafunzi mmepata madawati haya yatumieni vizuri kwenye matumizi
yaliyokusudiwa kwa lengo la kuwawezesha kufikia malengo yenu kwa
kuongeza ufaulu “Alisema. Kwa
upande wake Mkuu wa shule ya Sekondari Toledo Daudi Nchia alimshukuru
Waziri Ummy kwa msaada huo na kuongeza kuwa bado wanakabiliwa na
changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa matundu ya vyoo vya wasichana
.
Alisema kutokana na uhaba huo umesababisha wasichana na wavulana kushiriki katika huduma hiyo.
WAZIRI
wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ambaye
pia ni Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga{CCM) kulia akimkabidhi
madawati 40 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Toledo ya Jijini Tanga
Daudi Nchia ikiwa ni mkakati wake wa kukabiliana na uhaba uliopo
MTEKETA: NIMEFIKA DARAJA LA JPM KABLA SIJAFA

NA
MWANDISNHI MAALUM-KILOMBERO
MBUNGE
wa zamani wa Kilombero, Abdul Mteketa (CCM), ametimiza azma yake ya kutembelea
daraja jipya la Magufuli lililopo Wilayani Kilombero mkoani Morogoro.
Akizungumza
leo baada ya kutembelea daraja hilo, alisema yeye alikuwa ni moja ya viongozi
waliopigania ujenzi wa daraja hilo ukamilike haraka wakati Rais Dk. John
Magufuli alipokuwa Waziri wa Ujenzi katika Serikali ya awamu ya tatu.
“Kama
unavyojua katika maisha yangu ya kuumwa pengine nisingeliona hili daraja.
Lakini leo nimefika na kuona kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya awamu ya
tano chini ya Rais Dk. John Magufuli.
“Watu
wa Kilombero, Ulanga na Malinyi tunamshukuru kwa dhati kiongozi wetu mpendwa ambaye
amekuwa akifanya kazi kubwa y
“…tayari
umekamilisha ujenzi wa daraja na ameshaweka jiwe la msingi la ujenzi wa
barabara kutoka Kidatu hadi Ifaraka- Ulanga, sasa ametufuta machozi watu wa
Kilombero-Ulanga na kwa dhati ninampongeza Rais Magufuli,” alisema Mteketa
Akizungumza
hali yake ya kiafya, alisema anamshukuru Rais Magufuli kwani kwa sasa hali yake
imeimarika baada ya kupata msaada wa matibabu.
“Awali
nilikuwa na atembetea kwenye wheel chair lakini kwa sasa ninaweza
alau kusimama kwa msaada wa magongo. Sina la kusema zaidi ya kusema
asante Rais Magufuli nasi Watanzania tunakuombea kwa Mungu akupe afya njema ili
uweze kuongoza taifa letu kwa upendo kama unavyofanya sasa,” alisema
NA MWANDISHI
MAALUM, DODOMA
MBUNGE
wa Jimbo
la Dodoma Mjini Mh Anthony Peter Mavunde amewataka wananchi wa Jimbo la
hilo kushirikiana na serikali na Viongozi wao katika kujiletea maendeleo
na
kutoa wito kwa jamii kujitoa kwa dhati kuchangia maendeleo kama
wanavyofanya
kwenye shughuli mbalimbali za kijamii hasa katika sherehe mbalimbali
zikiwemo
harusi.
Mhe.
Mavunde ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana
na Ajira ameyasema hayo leo Agosti 25, 2018 wakati akiongoza mamia ya
wananchi wa kata ya Kikuyu-kusini
katika ujenzi wa vyumba vya madarasa Jijini Dodoma ambapo Mbunge huyo
amechangia matofali 1,000 na mifuko ya Saruji 130, Computer 1, Jezi,
mipira
pamoja na kusimika magoli ya chuma katika uwanja wa michezo uliopo
katika Shule ya
Msingi Kikuyu B.
Akimuunga mkono
Mhe. Mavunde, Mbunge wa Jimbo la Bahi Mhe. Omary Badwell amewapongeza wananchi wa
Kata ya Kikuyu Kusini kwa muitikio wao mkubwa kwenye shughuli za maendeleo na
kuahidi kushirikiana na Mhe. Mavunde kutatua changamoto za shule hiyo kwa kuchangia
mifuko 20 ya Saruji iliyopo eneo ambalo na yeye ni mkazi wake na watoto wake
pia wanasoma katika shule husika.
Aidha Diwani wa
kata ya Kikuyu Kusini Mhe. Kutika amemshukuru Mhe. Mbunge Mavunde kwa kusaidia kutatua
kero hiyo ya ukosefu wa vyumba vya madarasa na hivyo ujenzi huo utasaidia
kuboresha miundombinu ya shule hiyo na hivyo kuchukua wanafunzi wengi kwa wakati
mmoja.
Mhe. Mbunge akiwa na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya
Msingi Kikuyu B.
Mhe. Mavunde akikabidhi moja kati ya mifuko 130 ya saruji.








No comments :
Post a Comment