Chifu
Emmanuel Zulu Gama kutoka kabila la Wangoni Mkoani Ruvuma, akimwomba Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Dkt.Harrison Mwakyembe(hayupo pichani) ofisi yake kushiriki katika Tamasha la
Mashujaa waliyopigana Vita ya Majimaji linalofanyika kila Mwaka Mwezi Februari
mkoani Ruvuma, katika ufunguzi Mkutano wa Saba wa Umoja wa Machifu Tanzania
uliyofanyika leo katika Kijiji cha Marangu Mkoani Kilimanjaro.
Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe(katikati) akizungumza
wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa machifu ulioanza Agosti 26, 2018 huko
Marangu, mkoani Kilimanjaro.Pamona na mambo mengine, Dkt. Mwakyembe amewaagiza
Maafisa Utamaduni Mkoa na Wilaya nchini kukamilisha ukusanyaji wa maoni ya
wadau wa Sekta ya Utamaduni kwa ajili ya kuboresha Sera ya Utamaduni ya Mwaka
1997. Kushoto ni Mlezi wa Umoja wa Machifu Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu
Mhe.John Samuel Malecela na kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya
Utamaduni Bi.Lilian Beleko kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo.
Mwenyekiti
wa Umoja wa Machifu Tanzania Chifu Frank Marrialle (kushoto) akitoa ahadi ya
umoja huo kuwasilisha maoni yao kwa ajili ya kuboresha Sera ya Utamaduni ya Mwaka
1997 kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison
Mwakyembe(hayupo pichani) katika ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Umoja wa
Machifu Tanzania uliyofanyika leo katika Kijiji cha Marangu Mkoani
Kilimanjaro,kulia kwake ni Mlezi wa Umoja wa Machifu Tanzania Waziri Mkuu
Mstaafu Mhe.John Samuel Malecela.
Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe (kulia)
akikabidhi nakala 21 za Sera ya Utamaduni ya Mwaka 1997 kwa Mlezi wa Umoja wa
Machifu Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mhe.John Samuel Malecela (kushoto) katika
Ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Umoja wa Machifu Tanzania,uliyofanyika leo
katika Kijiji cha Marangu Mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kugawa kwa Machifu waliyoshiriki
Mkutano huo ili waweze kutoa maoni yao kutokana na mapungufu ya sera hiyo
inayofanyiwa marekebisho.
Chifu
Nshoma Hawa wa Ukamba Kahama akieleza
changamoto zinazomkumba katika ikulu yake ambapo ardhi ya himaya yake
iliyozikiwa machifu wenzake kuporwa na kugawiwa kwa wananchi kwa ajili ya
kilimo kinyume na utaratibu wa uhifadhi wa ardhi za makazi ya machifu kwa
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe (hayupo
pichani) katika Mkutano wa Saba wa Umoja wa Machifu Tanzania uliyofanyika leo
katika Kijiji cha Marangu Mkoani Kilimanjaro.
Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe aliyeketi
(watano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja
na baadhi ya Machifu wa Tanzania mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa
Saba wa Umoja wa Machifu Tanzania
uliyofanyika leo katika Kijiji cha Marangu Mkoani Kilimanjaro,wanne kulia ni
Mlezi wa Umoja wa Machifu Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mhe.John Samuel
Malecela,na wanne kulia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania Chifu Frank
Marrialle.
No comments :
Post a Comment