Wednesday, July 18, 2018

MAWASILIANO YAWEZESHA UKUSANYAJI WA MAPATO MOROGORO


JPEG. NA. 1
Naibu Waziri wa uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa tatu kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe S. Kebwe (wa pili kulia) picha ya maeneo yaliyojengwa minara ya mawasiliano na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) mkoani humo. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Mawasiliano Mhandisi Anjelina Madete na wa pili kushoto ni Mtendaji Mkuu wa UCSAF Mhandisi Peter Ulanga
JPEG. NA. 2
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro (aliyesimama) Dkt. Kebwe S. Kebwe akiongea na wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakati wa ziara yao ya kukagua hali ya mawasiliano mkoani humo. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye na wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Moshi Selemani Kakoso
JPEG. NA. 3
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu (aliyesimama katikati) akiuliza jambo kuhusu hali ya mawasiliano katika kijiji cha Kaole kilichopo wilayani Mvomero mkoani Morogoro wakiwa kwenye mnara wa Halotel wakati wa ziara yao ya kukagua hali ya mawasiliano mkoani humo. Wa pili kushoto ni Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye na wan nne kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Mhandisi Peter Ulanga
JPEG. NA. 4
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa ili kushoto) akifafanua jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakati wa ziara yao ya kukagua hali ya mawasiliano katika kijiji cha Kaole kilichopo wilayani Mvomero mkoani Morogoro. Wa tatu kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Moshi Selemai Kakoso na wa pili kulia ni Naibu Mkurugenzi wa Halotel, Morogoro
JPEG. NA. 5
Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Mhandisi Peter Ulanga akitoa taarifa ya upatikanaji wa mawasiliano mbele ya Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakati wa ziara yao mkoani Morogoro. Waliokaa mbele wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye, katikati ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Moshi Selemani Kakoso na anayefuata ni Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Kebwe S. Kebwe
JPEG. NA. 6
Mwenyekiti wa kitongoji cha Mchanga wa pwani Kaole kilichopo wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, Bwana Henry Daudi akiishukuru Serikali kwa kufikisha mawasiliano kwenye kijiji hicho wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Miundombinu ya kukagua upatikanaji wa mawasiliano mkoani humo. Wa kwanza kulia ni Naibu Mkurugenzi wa Halotel, Morogoro Bi……….Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Moshi Selemani Kakoso na wa tatu kulia ni Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Mhandisi Peter Ulanga
JPEG. NA. 7
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akiwa ndani ya gari lake akiongoza msafara wa wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Miundombinu ya kukagua upatikanaji wa mawasiliano katika kijiji cha Kaole kilichopo wilayani Mvomero mkoaani Morogoro
……………..
Ongezeko la upatikanaji wa huduma za mawasiliano yamechangia na kuwezesha ukusanyaji wa mapato ya Serikali katika maeneo mbali mbali nchini.
Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stevene Kebwe mbele ya
Kamati ya Bunge ya Miundombinu walipotembelea ofisini kwake wakati wa ziara yao ya kukagua hali ya mawasiliano mkoani humo. Dkt. Kebwe amesema kuwa kadri mawasiliano yanavyoongezeka yanawezesha ukusanyaji wa mapato mkoani humo ambapo hadi hivi sasa mkoa huo ni wa pili ukifuatiwa na mkoa wa Dar es Salaam.
Ameongeza kuwa anayaomba makampuni mengine ya simu kujitokeza na kujenga miundombinu ya mawasiliano ili kuongeza upatikanaji wa mawasiliano katika mkoa huo kwa kuwa kiasi cha asilimia 70 ya eneo la mkoa huo linapakana/linazungukwa na mbuga ya wanyama ya Selous. Pia, amefafanua kuwa mkoa wa Morogoro ni wa pili kwa ukubwa ukifuatiwa na mkoa wa Morogoro.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Moshi Selemani Kakoso amemueleza Dkt. Kebwe kuwa maeneo aliyonayo ya kiutawala katika mkoa huo ni makubwa.  Kakoso amesema kuwa kupitia Kamati anayoiongoza wataishauri Serikali ili kuhakikisha kuwa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inaongeza upatikanaji wa mawasiliano kwenye maeneo muhimu wanayoona muhimu  ya kiuchumi au ya kiusalama. Aidha, ametoa rai kwa wananchi wanaohujumu miundombinu ya mawasiliano kwa kuiba betri na sola kwenye minara ya mawasiliano waache mara moja na ameiomba Serikali ya mkoa huo kudhibiti jambo hilo.
Wakiwa kwenye kijiji cha Kaole kilichopo wilayani Mvomero mkoai Morogoro, Mhe. Kakoso ameipongeza Serikali kwa jitihada walizonazo kupitia UCSAF ya kufikisha mawasiliano sehemu mbali mbali nchini ambapo hakuna mvuto wa kibiashara ambapo wananchi wapatao 6,000 wanapata huduma za mawasiliano kwenye kijiji hicho. Pia, Ameongeza kuwa Kamati imebaini uwepo wa changamoto ya ulinzi kwenye miradi ya miundombinu ya mawasiliano, usafi na ukosefu wa mazingira rafiki kwenye maeneo hayo ambapo wakati wa kiangazi moto unaweza kutokea na kuharibu miundombinu hiyo.
Mhe. Kakoso ameiomba Serikali kupitia UCSAF kuhakikisha kuwa kunakuwa na mazingira rafiki ya ulinzi na usalama na usafi kwenye maeneo iliyojengwa miundombinu hiyo ikiwa ni pamoja na Serikali ya kijiji na wananchi kushirikiana kuilinda miundombinu hiyo. Amesema kuwa Serikali iweke utaratibu na mwongozo wa wa kuziwezesha Serikali za vijiji kupara mrabaha na kodi ili kunufaika na uwepo wa miundombinu ya mawasiliano kwenye maeneo yao.
Naye Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye amesema kuwa wako pamoja na Kamati kwenye ziara ya kukagua upatikanaji wa mawasiliano kwenye maeneo mbali mbali nchini ambapo tumeshuhudia Serikali ikitoa pesa nyingi za ili kujenga minara ya mawasiliano ili wananchi waweze kuwasiliana. Pia, amewaomba wananchi kuendelea kuilinda miundombinu ya mawasiliano iliyopo kwenye maeneo yao kwa kuwa imejengwa kwa manufaa yao.   
Mhandisi Nditiye ameilekeza UCSAF kuhakikisha kuwa minara iliyojengwa na kampuni ya simu ya Halotel ambayo haina miundombinu rafiki kwa walinzi ili waweze kukaa dani na kupata huduma ya choo waweze kujenga miundombinu hiyo ndani ya miwili nchi nzima.
Mtendaji Mkuuu wa UCSAF Mhandisi Peter Ulanga akifafanua suuala la changamoto za mazingira rafiki kwenye miundombinu ya mawasiliano amesema kuwa wanaishukuru Kamati kwa kufika kwenye maeneo hayo ili Serikali iendelee kuwawezesha na kuendelea kuboresha mazingira rafiki kwenye miundombinu hiyo.
Ameongeza kuwa hali halisi ya mawasiliano katika mkoa wa Morogoro ilikuwa ni kwa kiasi cha robo tu ya eneo la mkoa huo ambalo lilikuwa na huduma za mawasiliano ambapo hadi sasa katika kipindi cha miaka mitatu, UCSAF imefikisha mawasiliano katika kata 30 na wataendelea kuweka mawasiliano ili kupunguza kadhia ya mawasiliano katika maeneo mbali mbali ya mkoa wa Morogoro.
Amefafanua kuwa malengo ya UCSAF ni kufikisha mawasiliano kwenye kata 45 ambapo kuna changamoto kwa watoa huduma kujitokeza na kutekeleza miradi hiyo hivyo wataendelea kujifunza changamoto hizo na kuboresha zaidi.
Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Kaole kilichopo wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro Bwana Christopher Henry Daudi ameishukuru Serikali kwa kujenga minara a kufikisha huduma za mawasiliano. Amesema kuwa mnara wa Halotel uliopo kwenye kijiji hicho unatoa huduma za mawasiliano kwenye vijiji sita ambavyo ni Kaole yenyewe, Dihinda, Mziha, Khanga, Bwage na Disinga.

No comments :

Post a Comment